Sunday 14 February 2010

FA Cup: Bolton 1 Tottenham 1
Bolton na Tottenham itabidi zirudiane huko White Hart Lane baada ya kutoka suluhu 1-1 nyumbani kwa Bolton Reebok Stadium lakini Tottenham itabidi wajilaumu kwa kuukosa ushindi kwani walipewa penalti kipindi cha pili huku gemu ikiwa 1-1 iliyopigwa na Huddlestone lakini Kipa Jussi Jaaskelainen wa Bolton akaokoa.
Nahodha wa Bolton Kevin Davies ndie alifunga bao lao lililodumu hadi mapumziko lakini Jermaine Defoe akasawazisha kwa bomba kali kipindi cha pili.
Timu hizi zinategemewa kurudiana Februari 24.
Terry akiri makosa!!
Nahodha wa Chelsea John Terry amekubali kwamba yeye ndie alifanya makosa yaliyoruhusu bao zote mbili alizofunga Luis Saha Everton walipoibwaga Chelsea 2-1 hapo juzi huko Goodison Park.
Terry, alievuliwa Unahodha wa England kufuatia kashfa ya kutembea na gelfrendi wa Wayne Bridge aliekuwa Mchezaji mwenzake Chelsea, amepewa likizo fupi na Klabu yake ili apoze akili kufuatia skandali hilo na jana hakuwepo wakati Chelsea ilipoibamiza Cardiff 4-1 kwenye FA Cup.
Terry amewaomba radhi Mashabiki wa Chelsea kwa makosa yake na pia kwa kutokwenda upande wa jukwaa walilokaa Washabiki wa Chelsea huko Goodison Park kuwashkuru baada ya kipigo chao toka kwa Everton.
Terry ameahidi kuwa kuanzia sasa watahakikisha Wachezaji wote wanaenda kutoa shukrani kwa Washabiki baada ya mechi hata kama matokeo yakiwa mabaya.
Ferguson: Bora kucheza na Milan bila Kaka!
• Man United wako imara kwenda San Siro kuliko 2007
Sir Alex Ferguson amesema Manchester United haiwezi kutawaliwa na AC Milan Uwanjani San Siro kama ilivyotokea mwaka 2007 kwenye Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE waliyofungwa 3-0 na Kaka akiwa ndani ya Milan.
Manchester United watacheza na AC Milan hapo Jumanne huko San Siro kwenye mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na marudiano ni Machi 10 huko Old Trafford lakini safari hii Kaka hayuko tena na Timu hiyo kwani ameshahamia Real Madrid.
“Ni wakati muafaka kwenda San Siro.” Ferguson amesema. “Wikiendi hii wamecheza na kuifunga Udinese 3-2, wamempoteza Kaka na wana majeruhi! Sisi tumepumzika!”
Ferguson akaendelea kuongea kwa kuichambua AC Milan na kutamka kuwa imebadilika baada ya Kaka kuondoka na sasa wanatumia mfumo wa 4-3-3 huku Washambuliaji wakiwa Marco Borriello akiwa kati na pembeni mwake ni Ronaldinho kushoto na Pato kulia.
Pato hajacheza mechi hivi karibuni kwa sababu ya maumivu na Ferguson amesema ikiwa Pato hatocheza David Beckham atakuwa Winga ya kulia na itabidi wachunge krosi zake.
Ferguson amekiri kuumia kwa Giggs, alievunjika mkono, ni pigo lakini lakini amesema Timu yake nzima ni nzuri.

No comments:

Powered By Blogger