Tuesday 16 February 2010

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Leo ni Leo!!
[Saa 4 dak 45 usiku saa za bongo]
Jumanne, 16 Februar1 2010
AC Milan v Man U
Lyon v Real Madrid
Lyon v Real Madrid
Katika miaka mitano, mara ya mwisho ikiwa 2004, Real Madrid ambao wamewahi kuwa Mabingwa wa Ulaya mara 9, hawajawahi kutinga Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI na safari hii ili kuingia Robo Fainali ni lazima waitoe Timu ngumu ya Ufaransa Lyon wakiwa kwao Stade Gerland katika mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16.
Marudiano ni Machi 10 huko Uhispania, Uwanja wa Bernabeau.
Tangu wakati huo Real imetolewa katika hatua hii na Klabu za Juventus, Arsenal, Bayern Munich, Roma na mwaka jana na Liverpool.
Kwa Real Madrid kufika Fainali ni kitu muhimu mno kwa vile tu Fainali ya mwaka huu inafanyika nyumbani kwao Uwanja wao wa Bernabeau.
Kabla ya mechi ya leo, Real Madrid walishinda mechi yao ya La Liga majuzi walipoipiga Xerez bao 3-0 huku Cristiano Ronaldo, akitoka kifungo cha mechi mbili, akifunga bao 2.
Ushindi huo wa Real Madrid na kufungwa kwa Wapinzani wao FC Barcelona na Athletic Madrid kwenye Ligi Jumapili na kuwafanya wawe pointi 2 tu nyuma ya Barca kumewapa furaha kubwa Real na watataka furaha yao idumu kwa matokeo mazuri katika mechi na Lyon.
Real pia wana habari nzuri kwani Straika wao Karim Benzema waliemnunua kutoka Lyon aliekuwa kaumia sasa yuko fiti na tayari kuikabili Klabu yake ya zamani.
AC Milan v Manchester United
Leo katika Stadio Giuseppe Meazza, hilo ndio jina halisi la Uwanja ambao wengi tumeuzoea kama San Siro, AC Milan na Manchester United zitakumbana katika mechi ya kwanza ya UEFA CHAMPIONS LIGI huku marudio yakiwa Old Trafford Machi 10.
Kwa Wadau mvuto mkubwa wa mechi hii ni David Beckham, alie AC Milan kwa mkopo kutoka Klabu yake ya Marekani LA Galaxy, kucheza na Klabu yake ya zamani Manchester United ambayo aliihama mwaka 2003 kwenda Real Madrid kwa mara ya kwanza tangu ahame.
Mwenyewe Beckham amesema mechi hii na Man United si kisasi kwake kwani yeye bado ana mapenzi makubwa na Man United na pia mpaka leo anamtambua na kumuheshimu Sir Alex Ferguson kama Baba yake.
AC Milan, chini ya Kocha Mbrazil Leonardo, wanatoka kwenye ushindi wa jasho wa Serie A wa 3-2 dhidi ya Udinese walioupata Ijumaa na ushindi huo ulifuta uteja wa mechi 3 mfululizo kwenye Ligi.
Kwa Manchester United, ambao sasa wako kwenye wimbi la ushindi wakiwa washatinga Fainali ya Carling Cup baada ya kuwabwaga Mahasimu wao Manchester City na wapo pointi moja tu kwenye Ligi nyuma ya Chelsea huku Straika wao Rooney akifunga magoli kama mashine, wanaingia Uwanja wa San Siro kupambana na AC Milan kwa mara ya 4 wakiwa wamecheza nao mwaka 1958, 1969, 2005 na 2007 bila ya kumudu kufunga hata goli moja mara zote hizo!
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Kesho!!
[Saa 4 dak 45 usiku saa za bongo]
Jumatano, 17 Februari 2010
Bayern Munich v Fiorentina
FC Porto v Arsenal

No comments:

Powered By Blogger