Tuesday 16 February 2010

UEFA yabadili ratiba ili Wadau wafurahie!!
UEFA imesema ratiba ya mwaka huu ya mechi za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 imebadilishwa ili kutoa nafasi kwa Mashabiki wengi kuona mechi hizo laivu.
Mechi za kwanza za Raundi hii ya Mtoano zitaanza leo Februari 16 na kumalizika Februari 24 na marudiano yake ni kuanzia Machi 9 hadi Machi 17.
Wiki hii kuna mechi 4 yaani Jumanne mechi mbili na Jumatano mechi mbili na wiki ijayo ni hivyo hivyo yaani Jumanne mechi 2 na Jumatano mechi mbili.
Pia safari hii Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI itafanyika Jumamosi badala ya ile Jumatano tuliyoizoea na Fainali hiyo itafanyika Uwanja wa Real Madrid uitwao Bernabeau.
RATIBA NI:
Jumanne, 16 Februar1 2010
AC Milan v Man U
Lyon v Real Madrid
Jumatano, 17 Februari 2010
Bayern Munich v Fiorentina
FC Porto v Arsenal
Jumanne, 23 Februari 2010
Olympiakos v Bordeaux
VfB Stuttgart v Barcelona
Jumatano, 24 Februari 2010
CSKA Moscow v Sevilla
Inter Milan v Chelsea
MECHI ZA MARUDIANO:
Jumanne, 9 Machi 2010
Arsenal v FC Porto
Fiorentina v Bayern Munich
Jumatano, 10 Machi 2010
Man U v AC Milan
Real Madrid v Lyon
Jumanne, 16 Machi 2010
Chelsea v Inter Milan
Sevilla v CSKA Moscow
Jumatano, 17 Machi 2010
Barcelona v VfB Stuttgart
Bordeaux v Olympiakos
Bunduki 5 hazipo kwa Gunners!!!
• Ni Gallas, Almunia, Arshavin, Song & Eduardo nje!!!
Imethibitika kuwa Arsenal itawakosa Wachezaji wake watano kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI ya kesho wanayocheza Ureno na FC Porto kwa ajili ya kuumia.
Wachezaji hao ni Eduardo, Arshavin, Alex Song, Gallas na Manuel Almunia.
Tatizo kubwa la Arsenal litakuwa kwa Mafowadi kwani Robin van Persie ni majeruhi wa muda mrefu na hivyo itabidi wamtegemee Bendtner ambae ndio kwanza anarudi kutoka kuuguza majeraha yake ya muda mrefu.
Nafasi ya Gallas inaweza ikazibwa na Mkongwe Sol Campbell atakaeshirikiana na Thomas Vermaelen.
Nafasi ya Kipa Almunia itachukuliwa na Lukasz Fabianski.
FA yamtaka Warnock ajieleze kwa kutaka Refa Msaidizi afungiwe
Chama cha Soka England, FA, kimemtaka Meneja wa Crystal Palace Neil Warnock atoe maelezo kuhusu kauli yake aliyoitoa Jumapili mara baada ya sare ya 2-2 na Aston Villa ya mechi ya FA Cup Raundi ya 5 kwamba Refa Msaidizi alikosea kuwapa Aston Villa kona iliyozaa bao la pili la Villa la kusawazisha la dakika ya 87 na hivyo afungiwe kwa kosa hilo.
FA imempa Warnock wiki moja atoe maelezo yake ambayo ndiyo yataamua kama afunguliwe mashtaka au la

No comments:

Powered By Blogger