Wednesday 17 February 2010

Stoke City wanataka Viera asulubiwe!!
Tony Pulis, Meneja wa Stoke City, anataka Mchezaji wa Manchester City Patrick Viera aadhibiwe na FA kwa kosa la kumpiga teke Kiungo wao Glenn Whelan wakati Wachezaji hao walipoanguka chini baada ya kugombea mpira.
Tukio hilo lilitokea kwenye mechi ya jana ya Ligi Kuu iliyotoka sare 1-1 na Refa Alan Wiley hakuchukua hatua yeyote kwa Viera mbali ya kuongea nae.
Pulis anataka FA walitazame tukio hilo kwenye video baada ya Timu yake Stoke kuadhibiwa mwezi Oktoba mwaka jana pale Difenda wao Robert Huth alipofungiwa mechi 3 kwa kumpiga Beki wa West Ham Mathew Upson tukio ambalo Refa hakuliona na adhabu hiyo ilitolewa baada ya kuchunguzwa kwenye video.
Fellaini wa Everton nje msimu wote!!
Kiungo wa Everton Marouane Fellaini atakosa kipindi chote kilichobaki cha msimu huu baada ya kuthibitika ameumia vibaya enka kuliko ilivyokisiwa na maumivu hayo yamefananishwa na kama yale ya Straika wa Arsenal Robin van Persie.
Fellaini, miaka 22, aliumizwa na Beki wa Liverpool Sotirios Kyrgiakos hapo Februari 6 kwenye mechi ya Ligi ambayo Liverpool walishinda 1-0 licha ya kucheza pungufu baada ya Beki huyo kupewa Kadi Nyekundu kwa kumuumiza Fellaini.
Kyrgiakos sasa anatumikia adhabu ya kufungiwa mechi 3 kwa Kadi hiyo.

No comments:

Powered By Blogger