Saturday 20 February 2010

Man United yakung’utwa 3-1!
Baada ya kuipiga Chelsea 2-1 mechi iliyopita, leo Eveton imeitandika Manchester United 3-1 katika mechi ya Ligi Kuu.
Man United ndio walikuwa wa kwanza kufunga bao dakika ya 16 mfungaji akiwa Berbatov lakini Everton walisawazisha dakika 3 baadae kwa kigongo cha Bilyaletdinov.
Hadi mapumziko bao zilikuwa 1-1.
Everton walipata bao la pili kupitia Gosling alieingizwa kipindi cha pili na la tatu lilifungwa na Rodwell ambae pia aliingia kipindi cha pili.
Manchester United wanabaki nafasi ya pili nyuma ya Chelsea.
Vikosi vilivyoanza:
Everton: Howard, Baines, Heitinga, Distin, Neville, Bilyaletdinov, Donovan, Arteta, Pienaar, Osman, Saha.
Akiba: Nash, Yobo, Coleman, Gosling, Rodwell, Vaughan, Yakubu.
Man United: Van der Sar, Neville, Evra, Brown, Evans, Park, Carrick, Fletcher, Valencia, Berbatov, Rooney.
Akiba: Foster, Vidic, Rafael, Scholes, Gibson, Owen, Obertan
Refa: Howard Webb
LIGI KUU yaikata maini Pompey!!!
Ligi Kuu England imelikataa ombi la Portsmouth la kutaka kuruhusiwa kuuza Wachezaji licha ya Dirisha la Uhamisho kufungwa.
Portsmouth, wenye matatizo makubwa kifedha na Machi 1 wako Mahakamani wakitaka kufilisiwa na Mamlaka ya Kodi kwa kutokulipa Kodi, walitoa ombi hilo maalum ili haraka wapate fedha kukabiliana na kesi hiyo.
Inasadikiwa Portsmouth wana deni la Pauni Milioni 60.
Ingawa inaaminika FA na FIFA zilikuwa tayari kulikubali ombi la Portsmouth ili kukwepa madhara ya kufilisiwa kwa Portsmouth, Ligi Kuu ambayo ndiyo inaiendesha Ligi hiyo England imelikataa ombi hilo na imesema imetafakari kila kitu na imeona huu si muda muafaka kuwaruhusu Portsmouth kuuza Wachezaji.
Kwa mwaka kuna Madirisha mawili ya Uhamisho yanayotambulika na FIFA nayo ni lile la Januari 1 hadi 31 na la pili lile la Juni 1 hadi Agosti 31.

No comments:

Powered By Blogger