Friday 19 February 2010

LIGI KUU: Tathmini mechi za Jumamosi
Jumamosi, Februari 20
[saa 9 dak 45 mchana]
Everton v Manchester United
[saa 12 jioni]
Arsenal v Sunderland
West Ham v Hull City
Woves v Chelsea
[saa 2 na nusu usiku]
Portsmouth v Stoke City
Everton v Manchester United
Wayne Rooney anarudi Goodison Park uwanja alioibukia katika uchezaji wake kupambana na Klabu yake ya zamani Everton.
Rooney kwa sasa ni moto wa kuotea mbali na ameshafunga magoli 25 katika mechi zote alizocheza msimu huu na ndie aneongoza kwa ufungaji katika Ligi Kuu kwa kuwa na goli 21.
Lakini Everton pia wako kwenye fomu na katika mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu waliipiga Chelsea 2-1.
Lakini katika mechi hii Everton itawakosa Wachezaji wao mahiri Marouane Fellaini, Tim Cahill, Tony Hibbert na Phil Jagielka ambao ni majeruhi.
Nao Manchester United, endapo wakishinda mechi hii watachukua uongozi kwa vile Chelsea wanacheza baada ya mechi hii, itawakosa Nani na Rio Ferdinand ambao wako kwenye adhabu za kufungiwa na Ryan Giggs alievunjika mkono.
Katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu huko Old Trafford, Man United ilishinda bao 3-0.
Vikosi vinategemewa:
Everton (4-4-1-1): Howard; Neville, Distin, Yobo, Baines; Pienaar, Osman, Arteta, Donovan; Bilyaletdinov; Saha.
Man United (4-4-2): Van der Sar; Rafael, Evans, Brown, Evra; Scholes, Carrick, Fletcher, Park; Berbatov, Rooney.
Refa: Howard Webb.
Arsenal v Sunderland
Arsenal, wakitoka freshi kwenye kipigo cha Ureno mikononi mwa FC Porto, wanaikaribisha Uwanjani Emirates Sunderland ambayo imekuwa na matokeo mabaya na haijashinda katika mechi 12 lakini mechi yao ya mwisho kushinda ilikuwa ni ile waliyoifunga Arsenal.
Sunderland itawakosa Lee Cattermole na David Meyler, waliofungiwa, huku Kieron Richardson, Andy Reid, John Mensah, Fraizer Campbell, Anton Ferdinand, Jordan Henderson na Steed Malbranque ni majeruhi..
Arsenal huko Ureno walipofungwa na FC Porto iliwakosa Manuel Almunia, William Gallas, Alex Song, Eduardo na Andrei Arshavin lakini wote huenda wakacheza Jumamosi.
Vikosi vinategemewa:
Arsenal (4-3-3): Almunia; Sagna, Gallas, Vermaelen, Clichy; Fabregas, Song, Denilson; Nasri, Arshavin, Rosicky.
Sunderland (4-3-3): Gordon; Hutton, Turner, Kilgallon, McCartney; Malbranque, Cana, Zenden; Benjani, Bent, Jones.
Refa: Steve Bennett.
West Ham v Hull City
Hii ni mechi kati ya Timu zilizo chini kwenye msimamo wa Ligi zenye pointi sawa 24 ila West Ham iko juu ya Hull City kwa ubora wa magoli.
West Ham walikuwa hawajashinda katika mechi zao sita za nyuma lakini walishinda mechi yao ya mwisho.
Hull City wao msimu wote huu hawajashinda hata mechi moja ugenini.
Woves v Chelsea
Katika mechi yao ya mwisho kati ya Timu hizi Chelsea iliifunga vibaya Wolves kwa bao 4-0.
Baada ya kupigwa 2-1 na Everton katika mechi yao ya mwisho bila shaka Chelsea watakuwa mbogo katika mechi hii.
Vikosi vinategemewa:
Wolves (4-5-1): Hahnemann; Zubar, Craddock, Berra, Ward; Foley, Mancienne, Jones, Henry, Jarvis; Doyle.
Chelsea (4-4-2): Cech; Ivanovic, Terry, Carvalho, Zhirkov; Mikel, Ballack, Lampard, Malouda; Drogba, Anelka.
Refa: Kevin Friend.
Portsmouth v Stoke City
Timu taabani iliyo mkiani na yenye matatizo makubwa kifedha inaikaribisha Stoke City ambayo ina ahueni kubwa katika msimamo wa Ligi.
Kuanzia sasa, ili Portsmouth wapone kushuka Daraja, kila mechi kwao ni lazima iwe kama fainali au itakuwa baibai kwao.
MSIMAMO LIGI KUU England:
[Timu zimecheza mechi 26 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 58
2 Man Utd pointi 57
3 Arsenal pointi 52
4 Man City pointi 45 [mechi 25]
5 Liverpool pointi 44
6 Tottenham pointi 43
7 Aston Villa pointi 42 [mechi 25]
8 Birmingham pointi 37 [mechi 25]
9 Everton pointi 35 [mechi 25]
10 Fulham pointi 34
11 Stoke pointi 31 [mechi 25]
12 Blackburn pointi 31
13 Sunderland pointi 26 [mechi 25]
14 Wigan pointi 25 [mechi 25]
15 West Ham pointi 24 [mechi 25]
16 Wolves pointi 24 [mechi 25]
17 Hull pointi 24
18 Bolton pointi 23 [mechi 25]
19 Burnley pointi 23 [mechi 25]
20 Portsmouth pointi 16 [mechi 25]

No comments:

Powered By Blogger