Friday 19 February 2010

EUROPA LIGI: Liverpool, Fulham zashinda nyumbani
Bao la dakika ya 80 la David Ngog limeipa ushindi Liverpool wa bao 1-0 walipocheza kwao Anfield na Timu ya Rumania FC Unirea Urziceni.
Huko Craven Cottage, Fulham walitumia uwanja wa nyumbani vyema waliposhinda mabao 2-1 dhidi ya Timu ya Ukraine FC Shakhtar Donetsk ambao ndio wanaoshikilia Kombe la UEFA ambalo msimu huu limebadilishwa na kuwa EUROPA LIGI.
Bao la ushindi la Fulham lilifungwa na Bobby Zamora.
Mechi za marudiano zitakuwa ugenini wiki ijayo huko Rumania na Ukraine.
MATOKEO:
FC Rubin Kazan 3 v Hapoel Tel aviv 0
Ajax 1 v Juventus 2
Club Brugge 1 v Valencia 0
Villareal 2 v Wolfsburg 2
Standard Liege 3 v Red Bull Salzburg 2
FC Twente 1 v Werder Bremen 0
Lille 2 v Fenerbahce 1
Athletic de Bilbao 1 v Anderlecht 1
FC Kobenhavn 1 v Olympique de Marseille 2
Panathinaikos 3 v AS Roma 2
Atletico de Madrid 1 v Galatasaray 1
Fulham 2 v FC Shakhtar Donetsk 1
Liverpool 1 v FC Unirea Urziceni 0
Hamburger SV 1 v PSV Eindhoven 0
Hertha Berlin 1 v Benfica 1
Wolves yatwangwa Faini kwa kuchezesha Kikosi dhaifu!!
Klabu ya Ligi Kuu, Wolverhampton Wanderers, imetwangwa faini ya Pauni Elfu 25 kwa kuchezesha Kikosi dhaifu kwenye mechi ya Ligi waliyocheza Desemba 15 huko Old Trafford dhidi ya Manchester United na kufungwa 3-0.
Hata hivyo faini hiyo haitakiwi kulipwa kwa sasa.
Wolves ilibadili Wachezaji wote 10 wa mbele walipocheza na Man United siku 4 tu baada ya kuifunga Tottenham kwenye Ligi bao 1-0 na siku chache baada ya mechi ya Man United ilipanga tena Kikosi kamili na kuifunga Burnley 2-0.
Msemaji wa Ligi Kuu amesema hatua hiyo ya kuiadhibu Wolves imechukuliwa kwani ilikuwa ni kinyume kwa sheria za Ligi Kuu zinazotaka kila Timu kuchezesha Kikosi chao kamili.
Meneja wa Wolves Mick McCarthy amesema ameukubali uamuzi wa Ligi Kuu na yeye hakuwa na nia ya kuvunja sheria ila alichagua Kikosi ambacho alikiona ni sahihi kwa mechi na Man United.
Viera akubali kosa, kukosa mechi 3!!
Kiungo wa Manchester CityPatrick Vieira atazikosa mechi zijazo tatu za Manchester City baada ya kukubali kosa aliloshitakiwa na FA la kumpiga teke Glenn Whelan wa Stoke City kwenye mechi ya juzi ya Ligi na tukio hilo halikuadhibiwa na Refa.
FA ilichunguza video ya tukio na kuamua kumshitaki Viera.
Adhabu ya Viera inamaanisha atazikosa mechi za Manchester City dhidi ya Liverpool ya Jumapili, mechi ya FA Cup na Stoke City na ile ya Ligi na Chelsea.
Pompey waomba kibali kuuza Wachezaji
Portsmouth ambayo ina matatizo makubwa ya fedha imeomba kibali cha Ligi Kuu ili kuuza Wachezaji nje ya dirisha la uhamisho ili wakabiliane na matatizo yao ya kifedha yakiwa pamoja na kutaka kufilisiwa na Mamlaka ya Kodi kwa kutolipa kodi.
Hata hivyo ombi hilo la Portsmouth linahitaji kibali cha FIFA kwani madirisha ya uhamisho ni mawili tu nayo ni Januari 1 hadi 31 na jingine ni Juni 1 hadi Agosti 31.
Portsmouth wanasadikiwa kuwa na madeni ya kiasi cha Pauni Milioni 60 na hawajasema Mchezaji yupi anauzwa ingawa inaaminika Wachezaji Nadir Belhadj wa Algeria, Kevin Prince-Boateng na Marc Wilson ndio walengwa.
Msimu huu Portsmouth imeshamilikiwa na Matajiri wanne tofauti na wote wameshindwa kuinusuru balaa la kifedha linalosababisha hata Wachezaji kuchelewa kupata Mishahara na sasa ipo mkiani mwa Ligi Kuu hivyo kuandamwa na balaa la kushuka Daraja.

No comments:

Powered By Blogger