Thursday 18 February 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Porto, Bayern Munich zashinda nyumbani!!!
FC Porto imeifunga Arsenal mabao 2-1 huko Ureno na Bayern Munich, ikiwa nyumbani, imeipiga Fiorentina pia mabao 2-1.
Huko Ureno, FC Porto ndio ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia Varella lakini Sol Campbell wa Arsenal akasawazisha kwa kichwa.
Hadi mapumziko, Porto 1 Arsenal 1.
Porto ilipata bao la pili katika mazingira ya kushangaza kwani Beki Sol Campbell alitoa pasi ya nyuma kwa Kipa wake Fabianski na badala ya Kipa huyo kuupiga mpira huo mbele yeye akaudaka na Refa akaamua ipigwe frikiki isio ya moja kwa moja langoni kwa Arsenal.
Ndipo, kabla Arsenal hawajakaa vizuri, Ruben Micael haraka haraka akampasia Falcao aliefunga wakati Arsenal wameduwaa.
Huko Ujerumani, Bayern Munich iliitoa Fiorentina kwa bao 2-1 na bao la pili la Bayern lilifungwa na Miroslav Klose ambae alionekana waziwazi kuwa ofsaidi.
Katika mechi hii, Mchezaji wa Fiorentina Massimo Gobbi alipewa Kadi Nyekundu kwa kumchezea faulo Arjen Robben wa Bayern Munich.
Mechi za marudiano za Arsenal v FC Porto na Fiorentina v Bayern Munich zitafanyika Machi 9.
LIGI KUU: Wigan 0 Bolton 0
Katika mechi pekee ya Ligi Kuu siku ya Jumatano, huko KC Stadium, Timu zinazosuasua chini kwenye msimamo wa Ligi, wenyeji Wigan na Bolton zilitoka suluhu ya 0-0.
MECHI ZA LIGI KUU WIKIENDI HII:
Jumamosi, Februari 20
[saa 9 dak 45 mchana]
Everton v Manchester United
[saa 12 jioni]
Arsenal v Sunderland
West Ham v Hull City
Woves v Chelsea
[saa 2 na nusu usiku]
Portsmouth v Stoke City
Jumapili, Februari 21
[saa 11 jioni]
Aston Villa v Burnley
[saa 12 jioni]
Fulham v Birmingham
Man City v Liverpool
[saa 1 na robo usiku]
Wigan v Tottenham
Jumatatu, Februari 22
[saa 5 usiku]
Blackburn v Bolton

No comments:

Powered By Blogger