Thursday 18 February 2010

Leo ni usiku wa EUROPA LIGI!!!
• Mechi bwelele!!!
Leo kona mbalimbali za Ulaya zitawaka moto kwa mechi mbalimbali za EUROPA LIGI za Raundi ya Mtoano ya Timu 32.
Kuna mechi kadhaa tamu kama vile Ajax v Juventus, Villareal v Wolfsburg, Lille v Fenerbahce na kadhalika.
Timu za England, mbali ya Everton iliyocheza juzu na Sporting Lisbon na kushinda 2-1, zilizomo kwenye EUROPA LIGI ni Liverpool na Fulham.
Leo Liverpool itaikwaa FC Unirea Urziceni ya Romania wakiwa nyumbani Anfield.
Fulham pia wako nyumbani Craven Cottage na leo watacheza na FC Shakhtar Donetsk ya Ukraine.
RATIBA KAMILI:
FC Rubin Kazan v Hapoel Tel aviv
Ajax v Juventus
Club Brugge v Valencia
Villareal v Wolfsburg
Standard Liege v Red Bull Salzburg
FC Twente v Werder Bremen
Lille v Fenerbahce
Athletic de Bilbao v Anderlecht
FC Kobenhavn v Olympique de Marseille
Panathinaikos v AS Roma
Atletico de Madrid v Galatasaray
Fulham v FC Shakhtar Donetsk
Liverpool v FC Unirea Urziceni
Hamburger SV v PSV Eindhoven
Hertha Berlin v Benfica
Wenger alia na Refa kwa bao la Porto!!
Kufuatia kipigo cha bao 2-1 walichokipata jana huko Ureno, Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amedai FC Porto hawakustahili kupewa frikiki iliyozaa bao la pili na la ushindi kwa Porto kwa vile mpira alioudaka Kipa Lukasz Fabianski haukuwa pasi kwa Kipa ya kukusudia.
Wenger amedai: “Campbell alirudisha mpira kwa Kipa kwa bahati mbaya! Mpira ulimgonga Campbell na kwenda kwa Kipa.”
Lakini Wadau wanashangaa hata kama Campbell hakukusudia kwa nini Kipa Fabianski aliudaka wakati alikuwa na uwezo wa kuupiga.
Baada ya Refa kuamua ni frikiki, Porto, kabla Arsenal hawajajipanga, wakapasiana na kufunga kwa kushtukiza.
Hata goli la kwanza walilofungwa Arsenal Wadau wamemlaumu Kipa huyo kwa makosa.
Nahodha Cesc Fabregas wa Arsenal yeye hakuficha, alitoboa: “Magoli yote tuliyofungwa ni makosa ya kitoto! Silalamikii goli la pili, hata mie kama Mchezaji ningefanya vilevile na kupiga frikiki haraka!”
Alipohojiwa kuhusu makosa ya Kipa Fabianski, Arsene Wenger alikataa kumlaumu na alidai makosa yote yanapaswa kulaumiwa Timu nzima na si mtu mmoja.
Vidic ni utata!!
Kuna hali ya utata mkubwa kuhusu kuendelea kwa Nemanja Vidic kuchezea Manchester United huku kukiwa na habari nzito kuwa anadengua ili alazimishe kuihama Manchester United na kwenda Real Madrid au AC Milan.
Habari hizo zilipamba moto baada ya Vidic, alietegemewa kuwemo kwenye Kikosi cha Manchester United kilichosafiri kwenda Milan, Italia kucheza na AC Milan hapo Jumanne, kujitoa Kikosini dakika za mwisho na inadaiwa alifanya hivyo kwa madai bado hajawa fiti kucheza.
Ingawa Sir Alex Ferguson amekataa kuzungumza kwa undani kuhusu Vidic mbali ya kusema wanataka abaki Man United, hatima yake imekuwa gizani hasa baada ya Daktari wa Timu ya Taifa ya Serbia, Miodrag Mladenovic, kudai Manchester United haitaki kuwapa taarifa kuhusu maumivu ya Mchezaji huyo licha ya kuwaomba wajulishwe kwa vile Vidic ni muhimu kwa Timu ya Serbia.
Hata hivyo mwenyewe Vidic amedaiwa kusema yeye ni Mchezaji wa Manchester United hadi mkataba wake utakapoisha mwaka 2010 na hajazungumza na mtu yeyote kuhusu kuhama.
Kuhusu kutokucheza, Vidic amedai bado hayuko fiti na hawezi kujifosi tu kwani anaweza kujiletea madhara makubwa.
Kocha wa Serbia, Raddy Antic, amesema habari za kutokuwa fiti kwa Vidic ni kweli ingawa ataonekana uwanjani hivi karibuni.

No comments:

Powered By Blogger