Saturday 27 February 2010

Chelsea 2 Man City 4
• Bifu la Terry v Bridge: Bridge hakutoa mkono kwa Terry!!
Dunia nzima ilikaza macho kutaka kuona kama mwanzoni mwa mechi Wayne Bridge na John Terry watapeana mikono kufuatia skandali la Terry kutembea na gelfrendi wa Bridge lililozua Terry kufukuzwa Unahodha England na Bridge kugoma kuichezea England na dunia nzima ikaona Bridge hakutoa mkono huku mkono wa Terry ukielea hewani.
Pia dunia nzima ikashuhudia Manchester City wakiipa Chelsea, wakiwa nyumbani kwao Stamford Bridge, kipondo cha bao 4-2 kwenye mechi ya Ligi Kuu na kuwafanya wamalize mechi hii wakiwa mtu 9 tu baada ya Juliano Belleti na Michael Ballack kupewa Kadi Nyekundu katika nyakati tofauti na Refa Mike Dean.
Sasa uongozi wa Chelsea kwenye Ligi ni pointi moja tu mbele ya Manchester United.
Kwa ushindi wa leo Manchester City wamechukua nafasi ya 4 wakiwa pointi 3 mbele ya Tottenham.
Chelsea ndio waliopata bao mwanzo mfungaji akiwa Frank Lampard dakika ya 42 lakini dakika chache baadae Carlo Tevez alisawazisha kwa goli lilojaa vituko.
Goli hilo la Tevez lilianzia kwa Mikel Obi kupiga kichwa nyuma na Terry kuukosa mpira huo na kumfikia Tevez aliewahadaa Terry na Carvalho lakini akaparaza shuti lake huku Kipa Hilario nae akauparaza mpira kwa mkono na pole pole ukatiririka wavuni.
Kipindi cha pili Craig Bellamy akafunga bao la pili dakika ya 51 na Tevez akapachika bao la 3 dakika ya 76 kwa penalti iliyompa Kadi Nyekundu Belleti kwa kumchezea rafu Gareth Barry ndani ya boksi.
Bao la 4 la Man City lilifungwa na Bellamy kufuatia kaunta ataki kwenye dakika ya 86.
Chelsea walipata bao lao la pili dakika ya 90 kwa penalti aliyopiga Lampard baada ya Gareth Barry kumchezea rafu Anelka.
Vikosi:
Chelsea: Hilario, Ivanovic, Carvalho, Terry, Malouda, Ballack, Mikel, Lampard, Anelka, Drogba, Joe Cole.
Akiba: Turnbull, Paulo Ferreira, Kalou, Sturridge, Matic, Alex, Belletti.
Man City: Given, Richards, Kompany, Lescott, Bridge, Zabaleta, De Jong, Barry, Bellamy, Tevez, Adam Johnson.
Akiba: Taylor, Onuoha, Wright-Phillips, Santa Cruz, Sylvinho, Toure, Ibrahim.
Refa: Mike Dean

No comments:

Powered By Blogger