Monday 22 February 2010

Spurs wachukua nafasi ya 4
Tottenham Hotspurs, wakicheza ugenini Uwanja wa DW uliokuwa kama zizi la ng'ombe kwa jinsi ulivyojaa tope katikati kwa mvua kubwa, waliwafunga wenyeji wao Wigan bao 3-0 na kuchukua nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu sasa wakiwa na pointi 46 sawa na Manchester City lakini Spurs wana goli bora.
Nafasi za 5 hadi za 7 ni za Man City [pointi 46], Liverpool [pointi 45] na Aston Villa [pointi 45].
Jermaine Defoe ndie aliefungua kitabu cha Spurs kwa kuandika bao dakika ya 27 ingawa alionekana kuwa 'maili' moja ofsaidi.
Kipindi cha pili, Defoe alitolewa na kuingizwa Mrusi Roman Pavlyuchenko, ambae anadaiwa kutaka kuihama Spurs, na huyu ndie aliewaua kabisa Wigan pale alipopachika bao 2.
MECHI INAYOKUJA LIGI KUU:
Jumanne, Februari 23 [saa 5 usiku saa za bongo]
Man United v West Ham

No comments:

Powered By Blogger