Sunday 21 February 2010

Man City, Liverpool ngoma ngumu!!
Manchester City na Liverpool leo zimeshindwa kupata mbabe katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Uwanja wa City of Manchester walipotoka suluhu 0-0.
Mechi hii muda mwingi ilichezwa katikati na Makipa wote hawakupata hekaheka kubwa katika dakika zote 90.
Washabiki wa Liverpool watapata furaha kidogo baada ya kumuona Straika wao wa kutegemewa Fernando Torres akiingizwa mwishoni baada ya kutoonekana kitambo kutokana na kuwa majeruhi.
Vile vile Mchezaji mwingine wa Liverpool wa kutumainiwa, Yossi Benayoun, aliekuwa nje kwa muda sasa kwa tatizo la kuvunjika mbavu leo aliingizwa kipindi cha pili na hilo nalo litaleta faraja huko Anfield.
Nao Mashabiki wa Man City watakuwa wakiomba Straika wao Carlos Tevez arudi haraka kutoka kwao Argentina alikokwenda kwa matatizo ya kifamilia kwani Fowadi yao ilikosa kabisa uhai wa kuleta mikikimikiki ya kutafuta goli kama afanyavyo Tevez.
Fulham 2 Birmingham 1
Katika dakika ya 3 tu ya mchezo, Fulham wakiwa nyumbani Craven Cottage, walijikuta wako nyuma kwa bao walilojifunga wenyewe kupitia Mchezaji wao Baird.
Hadi mapumziko Fulham 0 Birmongham 1.
Kipindi Damien Duff alifumua shuti kwa guu lake la kushoto na kutingisha nyavu ikiwa ni dakika ya 59 na hivyo kufanya Fulham wawe sare.
Katika dakika ya 90, frikiki ya Bobby Zamora ilitinga na kuipa ushindi Fulham wa bao 2-1.
Timu hizi Fulham na Birmingham zimefungana zote zikiwa na pointi 37 lakini Fulham wako nafasi ya 9 na Birmingham wako ya 10 kwa ubora wao wa magoli.

No comments:

Powered By Blogger