Friday 26 February 2010

Jahazi latota Pompey lakini Wachezaji waungwana!!!
Meneja wa Portsmouth Avram Grant amesema Wachezaji wake wawili wamekubali punguzo la mishahara yao ili kuokoa ajira za Wafanyakazi wa kawaida wa Klabu hiyo yenye matatizo makubwa ya fedha na sasa iko chini ya Msimamizi maalum ili kuinusuru isitangazwe mufilisi.
Kwa kuwekwa chini ya Msimaizi maalum tayari Portsmouth imekiuka sheria za Ligi Kuu England na itakatwa pointi 9 na hilo, ni wazi, litaishusha Daraja kwani mpaka sasa wako mkiani na wana pointi 16 tu.
Grant amesema atakutana na Wachezaji wote ili kuongea jinsi ya kunusuru ajira za Wafanyakazi wa kawaida wengine.
Grant amenena: “Inasikitisha! Lakini tutakutana kuangalia nini tufanye tusaidie wengine!
Diouf: “Mimi ni dume!”
Mchezaji wa Blackburn Rovers anaetoka Senegal El-Hadji Diouf amechokoza hasira za Liverpool, Klabu aliyoihamia kutoka Lens ya Ufaransa mwaka 2002 na kukaa miaka mitatu, kwa kudai Blackburn itawafunga kirahisi Liverpool watakapocheza mechi ya Ligi Kuu Jumapili.
Diouf amedai: “Si ngumu kwenda Anfield na kuwafunga! Hapa England, kila Timu inaweza kuifunga nyingine! Utaona Timu kama Watford ishashuka Daraja lakini inaifunga Manchester United! Siogopi kuzomewa na kama sizomewi siwezi kucheza! Mie ni dume na ninahitaji kuonyesha watu mie ni dume!!”

No comments:

Powered By Blogger