Thursday 25 February 2010

EUROPA LIGI: Timu za England zipo ugenini leo!
Leo Ulaya yote ni mechi za marudiano za EUROPA LIGI na Timu 3 za England zilizomo kinyang’anyiro hicho zote zipo ugenini na zote zipo huko huku zikiwa na ushindi mwembamba wa mechi za kwanza.
Liverpool leo ipo Romania kucheza na Unirea Urziceni na inabidi waulinde ushindi wao wa bao 1-0 walioupata nyumbani kwao Uwanjani Anfield wiki iliyopita.
Nao Everton wako Ureno kucheza na Sporting Lisbon na wao pia inabidi waulinde ushindi wa bao 2-1 walioupata kwao Goodison Park wiki iliyopita.
Kwa Fulham, ambao wanacheza huko Ukraine watakaporudiana na Shakhtar Donetsk, hali ni hiyo hiyo ya kulinda ushindi wao wa bao 2-1 walioupata kwao Craven Cottage.
Mbali ya mechi ya Timu hizi 3 za England leo pia kuna mechi 12 nyingine za EUROPA LIGI.
Timu pekee ambayo tayari ishatinga Raundi inayofuata ya Mtoano ya Timu 16 ni Benfica ambayo juzi iliirarua Hertha Berlin bao 4-0 baada ya kutoka sare 1-1 mechi ya kwanza.

No comments:

Powered By Blogger