Wednesday 24 September 2008

Man United 3 Middlesbrough 1

Mabingwa wa LIGI KUU na Ulaya Manchester United jana waliifunga Middlesbrough 3-1 katika Uwanja wa Old Trafford na kuwatoa kwenye CARLING CUP.
Man U wakiwa na kikosi mchanganyiko wa chipukizi na maveterani waliutawala mchezo kabisa licha ya timu ya LIGI KUU Middlesbrough kushusha kikosi chao cha kwanza..
Mechi hii iliingia dosari kwenye kipindi cha pili dakika ya 66 pale Pogatetz wa Middlesbrough alipocheza rafu mbaya na kumuumiza vibaya kijana mdogo wa Brazil Kiungo wa Man U Rodrigo Possebon. Refa alimpa kadi nyekundu Pogatetz na Possebon alikimbizwa hospitali baada ya kuchanika mguu na kuna wasiwasi amevunjika pia.
Man Utd: Amos, Rafael Da Silva, Vidic, Brown, O'Shea, Nani, Possebon (Gibson 72), Anderson, Giggs (Manucho 84), Welbeck, Ronaldo (Tevez 61). AKIBA: Zieler, Cleverley, Gray, Eckersley.


MAGOLI: Ronaldo 25, Giggs 79, Nani 90.

Middlesbrough: Jones, Hoyte, Wheater, Pogatetz, Taylor, Downing, Digard (Riggott 72), O'Neil, Shawky (Adam Johnson 46), Aliadiere, Alves (Emnes 85). AKIBA: Turnbull, Arca, Walker, Craddock.
KADI NYEKUNDU: Pogatetz (66).
KADI YA NJANO: Adam Johnson.

GOLI: Adam Johnson 56.

WATAZAMAJI: 53,729

REFA: Andre Marriner (W Midlands).


No comments:

Powered By Blogger