Monday 22 September 2008


VITA DARAJANI:
CHELSEA 1 MAN U 1


=Scolari afurahia dro!

=Ferguson ajutia nafasi za magoli ya wazi!

Rekodi ya Chelsea ya kutofungwa nyumbani kwao Stamford Bridge imeendelea kubaki baada ya Mchezaji wao Kalou kuingizwa kutoka benchi na kusawazisha
katika dakika ya 80.
Man U ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika kipindi cha kwanza kwenye dakika ya 18 baada ya gonga safi sana kati ya Rooney, Berbatov na Evra na kisha mpira ukadondoka kwa Ji-sung Park aliemalizia.
Mabingwa wa LIGI KUU Man U walikuwa na uwezo wa kuongeza bao la pili lakini walipoteza nafasi za wazi kadhaa.
Baaada ya mechi, Meneja wa Chelsea Scolari alisema ameridhishwa na pointi hiyo moja waliopata hasa baada ya kupata pigo kwa kuumia Mchezaji wao wa kutuimaniwa Deco wakati akipasha joto kabla ya mechi kuanza.
Nae Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson amesema hii ilikuwa nafasi murua ya kuwafunga Chelsea ila kosa lao la kupoteza nafasi za wazi za magoli ndilo liliwaua.
Chelsea: Cech, Bosingwa, Carvalho (Alex 12), Terry, Ashley Cole, Obi, Joe Cole, Ballack (Kalou 74), Lampard, Malouda (Drogba 46), Anelka.AKIBA: Cudicini, Bridge, Belletti, Ferreira.
KADI: Obi.
GOLI: Kalou 80.
Man Utd: Van der Sar (Kuszczak 32), Neville, Ferdinand, Evans, Evra, Fletcher, Hargreaves, Scholes (Ronaldo 55), Park (O'Shea 75), Berbatov, Rooney.Subs Not Used: Brown, Giggs, Nani, Tevez.
KADI: Scholes, Ferdinand, Neville, Berbatov, Rooney, Evra, Ronaldo.
GOLI: Park 18.
WATAZAMAJI: 41,760
REFA: Mike Riley (Yorkshire).

No comments:

Powered By Blogger