Friday 26 September 2008



KOMBE LA CARLING:
DRO YA MECHI ZA RAUNDI YA 4 KUFANYIKA KESHO JUMAMOSI 27 SEPTEMBA 2008
Dro ya kuamua timu zipi zinakutana kwenye RAUNDI YA 4 ya KOMBE LA CARLING itafanyika kesho Jumamosi tarehe 27 Septemba 2008.
Timu 16 zimeingia Raundi hii ya 4 zikiwa Timu 9 toka LIGI KUU na Timu 7 toka Daraja la Chini yake.
Timu za LIGI KUU ni Tottenham, Chelsea, Wigan, Blackburn, Liverpool, Sunderland, Stoke City, Man U na Arsenal.
Timu za Daraja la chini ni QPR, Brighton, Burnley, Leeds, Rotherham, Swansea na Watford.
Mechi za Raundi ya 4 zitachezwa wiki ya kuanzia Desemba 1, 2008.
Washindi wanane toka Raundi hiyo ya 4 watasonga kwenye Raundi ya 5 na washindi wa Raundi hii wanaingia Nusu Fainali itakayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Fainali ya CARLING CUP itafanyika tarehe 1 Machi 2009.

No comments:

Powered By Blogger