Thursday 25 September 2008

CROATIA WAPIGWA FAINI KWA KUWA WABAGUZI

FIFA kimewapiga faini Croatia kwa kosa la washabiki wao kuwa wabaguzi wa rangi katika mechi yao na Uingereza iliyochezwa mapema mwezi huu mji mkuu wao Zagreb ya kutafuta nchi zitakazoingia Fainali Kombe la Dunia 2010 huko Afrika Kusini mechi ambayo Croatia ilishindiliwa 4-1 na kupoteza rekodi yao ya kutofungwa nyumbani.
Ubaguzi huo ulifanywa na kikundi kidogo cha watazamaji kilichotoa sauti kama nyani kila Mshambuliaji wa Uingereza Emile Heskey [pichani] alipopata mpira.
Chama cha Mpira cha Uingereza kililalamika FIFA kwa kitendo hicho na sasa FIFA imeitwanga Croatia faini ya takriban Shilingi za bongo milioni 30.
Hii ni mara ya pili kwa Croatia kupatikana na hatia na kulimwa faini kwa kosa kama hili.
Katika mechi ya Robo Fainali ya EURO 2008 na Uturuki washabiki wa Croatia walileta ubaguzi na wakapigwa faini.
Sasa FIFA imewapa onyo la mwisho na endapo kosa hili litatokea tena basi watafungiwa.

No comments:

Powered By Blogger