Friday 26 September 2008

CARLTON COLE WA WEST HAM AKAMATWA AKIENDESHA GARI AKIWA NJWIII!

Mshambuliaji wa West Ham, Carlton Cole, umri miaka 24, alikamatwa na Polisi usiku wa manane wa Jumanne akiendesha gari katikati ya jiji la London huku akiwa amelewa chakari.
Alipokamatwa tu akapimwa hapohapo kwenye tukio kiwango cha pombe kilichopo mwilini kisha akapelekwa kituoni.
Baadae akaachiwa kwa dhamana.
Usiku wa Jumanne hiyo ya tukio timu yake ya West Ham ilifungwa na Watford bao 1-0 kwenye Mechi ya Kombe la Carling.
Wakati kesi yake ikiendelea kuchunguzwa itabidi arudi tena Polisi mwezi Novemba ili dhamana yake iendelee.

No comments:

Powered By Blogger