Saturday 27 September 2008

UEFA CUP KUITWA EUROPA LEAGUE MSIMU UJAO

Kuanzia mwakani, hasusan msimu ujao wa soka, UEFA CUP ambalo hushindaniwa na Klabu za Ulaya ambazo hazikufuzu kuingia UEFA CHAMPIONS LEAGUE na kujumuishwa na Klabu zilizoshika nafasi ya tatu kwenye Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE, litabadilishwa jina na kuitwa EUROPA LEAGUE.

Vilevile mtindo wa uchezaji utabadilishwa kutoka wa sasa wa mtoano na kuanzishwa mtindo wa ligi kama ilivyo kwa UEFA CHAMPIONS LEAGUE. Mfumo huu wa ligi utakuwa na jumla ya Klabu 48 zitakazogawanywa makundi 12 ya timu nne nne kila moja ambazo zitacheza kwa mtindo wa ligi wa mechi za nyumbani na ugenini.

Washindi wawili wa juu wa kila Kundi watajumlishwa na timu 8 zilizoshika nafasi ya tatu kwenye Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kufanya jumla ya timu 32 zitakazocheza kwa mtoano hadi kufikia Fainali.

No comments:

Powered By Blogger