Friday 26 September 2008

BRAZIL WATAJA KIKOSI CHAO CHA MECHI ZA MTOANO KOMBE LA DUNIA

-KAKA, ROBINHO NDANI, RONALDINHO NJE!

Kocha wa Brazil ameteua kikosi cha Wachezaji 22 watakaocheza mechi za mtoano wa KUNDI LA NCHI ZA MAREKANI KUSINI kuwania kuingia FAINALI KOMBE LA DUNIA AFRIKA KUSINI 2010 ambapo watacheza mechi mbili mwezi ujao Oktoba.

Tarehe 12 Oktoba 08 Brazil inapambana na Venezuela na siku nne baadae inacheza na Colombia.

Dunga amemrudisha kikosini Kaka ambae hajachezea Timu ya Taifa tangu Novemba mwaka jana. Ronaldinho, ingawa aliiwakilisha Brazil kwenye Olympic huko Beijing akiwa Nahodha, ametupwa nje kwa kile Dunga alikiita kukosa nafasi ya kucheza mechi nyingi na Klabu yake mpya ya AC Milan.Wachezaji wapya wa Manchester City Jo na Robinho wamo kwenye kikosi hicho pamoja na Anderson wa Manchester United.

KIKOSI KAMILI [KLABU WANAZOTOKA]

MAKIPA: Julio Cesar (Inter Milan), Doni (AS Roma) WALINZI: Maicon (Inter Milan), Daniel Alves (Barcelona), Lucio (Bayern Munich), Juan (AS Roma), Thiago Silva (Fluminense), Alex (Chelsea), Kleber (Santos), Juan (Flamengo) VIUNGO: Gilberto Silva (Panathinaikos), Josue (Wolfsburg), Lucas (Liverpool), Anderson (Manchester United), Elano (Manchester City), Kaka (AC Milan), Mancini (Inter Milan/ITA), Julio Baptista (AS Roma/ITA) WASHAMBULIAJI: Luis Fabiano (Sevilla), Jo (Manchester City), Pato (AC Milan), Robinho (Manchester City)

No comments:

Powered By Blogger