Thursday 25 September 2008



Baada ya kitimtim cha Kombe la CARLING cha jana Jumatano na juzi Jumanne macho yote sasa yako kwenye LIGI KUU UINGEREZA itakayowaka moto Jumamosi na Jumapili kwa jumla ya mechi 10 ikimaanisha timu zote 20 za LIGI KUU zitakuwa zikicheza.
Mechi kubwa wikiendi hii bila shaka ni ile inayowakutanisha WATANI WA JADI wanaotoka mji mmoja mji wa Liverpool.
Kwa kuwa mechi hii ina ushindani mkubwa na hulifanya jiji lote la Liverpool lizizime na kupambwa kwa bendera za bluu kwa upande mmoja na nyekundu kwa upande mwingine inachezwa jua utosini saa sita dak 45 mchana kwa saa za huko kwa matakwa ya POLISI wa mji huo wa Liverpool. Bongo itakuwa saa 8 dak 45 mchana.
Mechi hii ni pambano kati ya Everton na Liverpool litakalochezwa Uwanja wa Goodison Park.


RATIBA KAMILI YA WIKIENDI:
Jumamosi, 27 Septemba 2008 Saa ni za bongo]

Everton v Liverpool [saa 8 dak 45 mchana];

Aston Villa v Sunderland [saa 11 jioni];

Fulham v West Ham [saa 11 jioni];

Man U v Bolton [saa 11 jioni];

Middlesbrough v West Brom [saa 11 jioni];

Newcastle v Blackburn [saa 11 jioni];

Stoke City v Chelsea [saa 11 jioni];

Arsenal v Hull City [saa 1 na nusu usiku];

Jumapili, 28 Septemba 2008

Portsmouth v Tottenham [saa 9 na nusu mchana];

Wigan v Man City [saa 12 jioni];

No comments:

Powered By Blogger