Tuesday 23 September 2008


'ZAKUMI': chui ambae ndie katuni rasmi wa KOMBE LA DUNIA AFRIKA KUSINI 2010!


Chui mwenye nywele 'AFRO' za rangi ya kijani ametambulishwa rasmi kama ndie atakuwa 'KATUNI' rasmi wa mashindano ya FAINALI za KOMBE la DUNIA AFRIKA KUSINI 2010 na amepewa maalum jina na tarehe yake ya kuzaliwa.


Katuni huyu ataitwa 'ZAKUMI' na tarehe yake ya kuzaliwa ni 16 Juni 1994.
Maana ya jina lake ni: Herufi mbili za kwanza 'ZA' ni kifupi cha jina la nchi yaani SOUTH AFRICA kwa lugha ya Afrikaans ambayo ni moja ya lugha 11 rasmi za nchi ya Afrika Kusini na 'KUMI' maana yake ni 10 kwa lugha nyingi za Kiafrika huko kusini na inamaanisha mwaka 2010 ambao ni mwaka wa FAINALI hizo.


Tarehe rasmi ya kuzaliwa ZAKUMI, 16 Juni 1994, ndio siku ambayo UBAGUZI WA RANGI huko Afrika Kusini ulitokomezwa rasmi.


Tarehe hii kwa sasa husheherekewa kila mwaka kama SIKU YA VIJANA ikiashiria machafuko ya Soweto ya mwaka 1976 wakati waandamanaji vijana walipoleta pigo kubwa kwa utawala dhalimu wa kibaguzi wa Weupe wachache huko Afrika Kusini.


Msemaji wa Kamati ya Maandalizi ya fainali hizo Tim Modise, wakati wa utambulisho rasmi ambako mtu alievaa guo linalofanana na ZAKUMI alicheza danadana na Mark Fish mchezaji wa zamani wa Afrika Kusini aliewasaidia kunyakua Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1996, alitamka: 'ZAKUMI hapa Afrika Kusini kwa lugha nyingi zetu za wenyeji ina maana 'NJOO HAPA''.


Nae mbunifu wa ZAKUMI, Andries Odendaal wa Cape Town, Afrika Kusini amesema nwele za kijani za chui huyu zinamaanisha nyasi za uwanja wa mpira.
FIFA walibuni mtindo wa kuwa na KATUNI mahsusi wa kila FAINALI za KOMBE la DUNIA mwaka 1966 wakati fainali zikifanyika Uingereza kwa kuwa na simba alievaa bendera ya Uingereza alieitwa Willie.


Wengine walikuwa Naranjito wa Spain mwaka 1982 aliekuwa na umbo la chungwa, mwaka 1990 huko Italia alikuwepo katuni mwenye shepu ya vijiti alievaa bendera ya Italia iliyokuwa na alama ya 'kwaheri' na Footix alikuwa jogoo wa Kifaransa mwenye rangi za bendera ya Ufaransa kwa fainali zilizochezwa nchi hiyo mwaka 1998.

No comments:

Powered By Blogger