Saturday 27 September 2008



KILIO ARSENAL SIKU WENGER ANAYOSHEHEREKEA MIAKA 12 KUWA HAPO!!

Arsenal 1 Hull City 2

Leo ni siku ya kuadhimisha miaka 12 tangu Arsene Wenger awe Meneja wa Arsenal lakini imekuwa siku ambayo atataka aisahau haraka baada ya kupata kipigo cha mabao 2-1 nyumbani kwake Emirates Stadium tena toka timu 'kibonde' Hull City iliyopanda Daraja msimu huu kwa mara ya kwanza tangu ianzishwe.

Vilevile Hull City imekuwa timu ya pili kuwafunga Arsenal kwenye LIGI KUU hapo kwao Emirates Stadium tangu uwanja huo mpya uanze kuchezewa.

Timu ya kwanza kuifunga Arsenal kwenye mechi ya LIGI KUU hapo Emirates ni West Ham waliposhinda bao 1-0 lililofungwa na Mchezaji wao Bobby Zamora katika mechi iliyochezwa Aprili, 2007. Tangu siku hiyo mpaka kipigo cha leo Arsenal imecheza mechi 25 za LIGI KUU bila kupoteza mechi.

Hadi mapumziko mechi ilikuwa suluhu ya 0-0. Kipindi cha pili kuanza Arsenal walipata bao walilojifunga wenyewe Hull City. Mbrazil Giovanni alisawazishia Hull City kwa kiki kali ya kistadi sana na Mshambuliaji Cousin akawapatia Hull City bao la ushindi kwa kichwa baada ya kona.

No comments:

Powered By Blogger