Saturday 27 September 2008

KINDUMBWENDUMBWE CHA MJI WA LIVERPOOL: Everton 0 Liverpool 2

Magoli mawili ya Fernando Torres ya kipindi cha pili yaliwapa ushindi Liverpool wakiwa ugenini Uwanja wa Goodison Park nyumbani kwa Everton kwenye kitimtim cha wenyeji wawili wa mji wa Liverpool ambao ni watani wa jadi.

Magoli hayo yalifungwa katika muda usiozidi dakika 4 kati yake na yaliwavunja nguvu Everton ambao mara tu baada ya mabao hayo mchezaji wao Tim Cahill alipewa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu mbaya Kiungo wa Liverpool Xabi Alonso.

Everton pengine watalalamika sana kwa kunyimwa penalti ya wazi kipindi cha kwanza baada ya Mshambuliaji wao Yakubu kusukumwa kwa makusudi ndani ya boksi.

No comments:

Powered By Blogger