Sunday 21 September 2008


MAN CITY WAWABAMIZA PORTSMOUTH!


Wakati BIG MECHI kati ya CHELSEA v MAN U imeisha 1-1, leo MAN CITY wakiwa nyumbani waliwashindilia Portsmouth 6-0 na huu ni ushindi mkubwa wa kwanza tangu LIGI KUU ianze msimu huu.
Wafungaji wa Man City ni Jo, Richard Dunne, Robinho, Shaun Wright-Phillips na Ched Evans.

Katika mechi nyingine, Everton wakiwa ugenini wakicheza nyumbani kwa Hull City, walikuwa nyuma kwa bao 2-0, waliibuka na kurudisha na ngoma ikawa 2-2.
Magoli ya Hull City yalifungwa na Michael Turner kufuatia kona na la pili lilimbabatiza Nahodha wa Everton Phillip Neville na Kipa Tim Howard na kuingia.
Kipindi cha pili Everton walimwingiza Luis Saha kuchezea mechi yake ya kwanza tangu ahamie Everton kutoka Man U lakini walikuwa Tim Cahill aliepata bao la kwanza kwa Everton na kazi nzuri ya Luis Saha ilimfanya Leon Osman asawazishe.

Nao Tottenham Hotspurs wameendelea kusuasua baada ya kutoka dro ya 0-0 nyumbani walipocheza na Wigan.
Baada ya mechi 5 Tottenham wamepiga nanga kama timu ya mwisho kwenye msimamo wa LIGI KUU.

No comments:

Powered By Blogger