Thursday 25 September 2008

MATOKEO CARLING CUP: MECHI ZA JUMATANO 24 SEPTEMBA 2008

Timu za LIGI KUU Aston Villa na Manchester City zimeaga CARLING CUP baada ya kubwagwa na timu za Daraja la Chini za QPR na Brighton.
Aston Villa ikiwa nyumbani kwake ilipigwa bao 1-0 na QPR.
Manchester City wakicheza ugenini nyumbani kwa Brighton walikwenda sare ya 2-2 katika dakika 90 na muda wa nyongeza wa nusu saa haukupata mshindi ndipo tombola ya penalti ikawapa ushindi Brighton wa mabao 5-3.
Nayo timu isiyokuwa na Meneja, Newcastle, ilipata pigo jingine baada ya kupigwa nyumbani mabao 2-1 na Tottenham.
Chelsea walionyesha ubabe pale walipowabamiza Portsmouth waliokuwa wakicheza nyumbani kwa mabao 4-0.
Katika mechi nyingine Wigan wanaocheza LIGI KUU waliibwaga Ipswich inayocheza Daraja la Chini mabao 4-1 licha ya Ipswich kuwa uwanja wa nyumbani.

Blackburn wakiwa nyumbani Ewood Park waliwatoa wenzao kwenye LIGI KUU Everton kwa bao 1-0.


No comments:

Powered By Blogger