Sunday 21 September 2008


MECHI YA LIGI KUU:
CHELSEA v MAN UNITED
==utambi wazidi kupulizwa!!


Sir Alex Ferguson amezidi kuchochea moto unaofukuta kwa mechi ya kesho baada ya kutoa kauli ya mzaha kuhusu Manchester United kurudi tena kucheza Uwanja wa Chelsea Stamford Bridge wakati alipokumbusha jinsi Wachezaji wake hasa Patrice Evra alivyokashifiwa, kutukanwa na kushambuliwa na Wasimamizi wa kukata nyasi za uwanja huo walipokwenda kucheza mechi msimu uliokwisha.
Ugomvi huo uliibuka mara baada ya mechi kwisha wakati Wachezaji wa Man U ambao hawakucheza mechi hiyo walitakiwa wakapashe joto uwanjani.
Wachezaji hao walikuwa ni Patrice Evra, Scholes, Tevez na Park.
Lakini walipoanza mazoezi yao wakisimamiwa na Mkufunzi wa Mazoezi wa Man U wakatokea wakata majani wa uwanja huo wa Chelsea na kuwatukana huku wakimpakia matusi ya ubaguzi Evra kwa sababu ni mweusi.

Mara ya mwisho kuja kucheza Stamford Bridge ilikuwa msimu uliokwisha ambao Man U walikuwa wanaongoza ligi na wakateremsha kikosi wengi wanadhani ni 'hafifu' ingawa bao la penalti la ya utata ndio liliwapa ushindi Chelsea ambao hata hivyo ushindi huo haukuwasaidia wao Chelsea kunyakua ubingwa.
Man U ndie alieibuka bingwa.

Kwa sasa kuna kesi FA inayowahusu Wasimamizi wa uwanja wa Chelsea na Patrice Evra.

Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson akakejeli:'Mara ya mwisho wakata nyasi walitushambulia, sasa hatujui Jumapili wameweka nini! Labda tutakuta katapila la kuvunia!'

Ferguson hakuishia hapo bali aliongeza:'Kama utatazama na kukumbuka miaka 12 au 13 ya LIGI KUU, nani ulimuona? Arsenal v Manchester United, Manchester United v Arsenal! Ndio, kwa sasa tuna Chelsea lakini historia ya Arsenal na Manchester United unazungumzia historia za klabu hizo ambazo ni historia za kweli! Sasa hao Chelsea ndio kwanzaaa wanaanza historia sisi na Arsenal tushatengeneza!!'

Ferguson akazidi kupiga msumari: 'Hawana tofauti na msimu uliokwisha! Tofauti ni kwamba hawana tena kwenye kiungo ile miguvu ya Makelele au Essien, wana Deco mchezaji mdogo, mjanja, mchezaji mzuri na hilo limesababisha tofauti ndogo ya uchezaji wao!'

No comments:

Powered By Blogger