Wednesday 24 September 2008


CARLING CUP: MATOKEO YA MECHI ZA JUMANNE 23 Septemba 2008


Timu za LIGI KUU Fulham na West Ham jana zilipigwa vikumbo na timu za Daraja la chini na kutolewa nje ya CARLING CUP.
Fulham ilifungwa 1-0 na Burnley wakati Watford iliipa West Ham kipigo hichohicho cha bao 1-0.
Vigogo Man U, Arsenal na Liverpool wote walishinda. Chelsea anacheza leo usiku.
Timu nyingine za LIGI KUU zilizonusurika kutolewa ni Sunderland na Stoke City ambazo zilijitutumua hadi muda wa nyongeza na kisha kushinda timu za Darala chini kwa mikwaju ya penalti.
Sunderland ilikuwa magoli mawili nyuma zidi ya Northamton Town lakini iksawazisha na kwenda muda wa nyongeza ambao haukutoa mshindi. Hivyo mikwaju ya penalti ikawapa ushindi Sunderland wa 4-3.
Nao Stoke City pia walitoka dro 2-2 na Reading mpaka wa muda wa nyongeza kwisha na wakashinda kwa mikwaju ya penalti 4-3.

Arsenal 6 Sheffield United 0

Timu ya Arsenal uwanjani kwao Emirates na kikosi cha chipukizi waliibamiza timu ya Daraja la chini ya LIGI KUU Sheffield United mabao 6-0 kwenye mtoano wa CARLING CUP.
Hivyo Arsenal wanasonga mbele kuingia raundi ya nne.
Arsenal: Fabianski, Hoyte, Djourou, Song Billong (Lansbury 70), Gibbs, Randall, Ramsey, Merida (Coquelin 71), Wilshere, Bendtner (Simpson 71), Vela.
AKIBA: Mannone, Emmanuel-Thomas, Ogogo, Frimpong.
MAGOLI: Bendtner 31, 42, Vela 44, 50, Wilshere 57, Vela 87.
Sheff Utd: Kenny, Halford, Morgan, Kilgallon, Naysmith, Cotterill (Naughton 46), Speed (Hendrie 73), Quinn, Montgomery, Beattie (Robertson 76), Webber.
AKIBA: Bennett, Sharp, Geary, Ehiogu.
KADI: Halford.
REFA: Phil Dowd (Staffordshire).
WATAZAMAJI: 56,632

No comments:

Powered By Blogger