Sunday 21 September 2008

FERGUSON v SCOLARI: mara ya pili timu timu zinazoongozwa na wao kukwaana!!


Leo saa kumi jioni saa za bongo Chelsea wanawakaribisha uwanjani kwao Stamford Bridge mjini London Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United katika pambano linalongojwa kwa hamu dunia nzima.
Wengi wanahisi pambano hili ni kati ya timu zinazotegemewa kunyakua ubingwa wa LIGI KUU ingawa vilevile Liverpool na Arsenal pia zimo kundi hilo.
Pambano hili la leo linakutanisha Mameneja wazoefu sana kwa mara ya kwanza kwenye mechi ya LIGI KUU.
Pengine wengi hawajui kuwa hii ni mara ya pili kwa timu zinazoongozwa na Sir Alex Ferguson na Luiz Felipe Scolari kupambana uso kwa uso.
Mara ya kwanza ilikuwa mwishoni mwa mwaka 1999 wakati Sir Alex Ferguson alipoingoza Manchester United wakati huo ikiwa ni Bingwa wa Klabu za Ulaya kupambana na Klabu ya Brazil Palmeiras ambayo ilikuwa Klabu Bingwa ya Nchi za Marekani Kusini ikiongozwa na Meneja Luiz Felipe Scolari katika pambano la kugombea Kombe la Mabara huko Tokyo, Japan.
Bao la Nahodha Roy Keane kufuatia krosi ya Ryan Giggs liliwapa Kombe hilo Manchester United.
Alipoulizwa Scolari kama anakumbuka hilo alijibu: 'Nakumbuka wakati Ferguson akipanda jukwaani kupokea kombe mie nilikuwa tayari nimeyayuka!'

No comments:

Powered By Blogger