Wednesday 24 September 2008


FERGUSON AFOKA KUHUSU KUUMIZWA CHIPUKIZI WAKE

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amekuja juu kuhusu kuumizwa kwa Kiungo chipukizi wake Rodrigo Possebon kutoka Brazil mwenye umri wa miaka 19 katika mechi ya jana ya KOMBE LA CARLING ambayo Man U waliifunga Middlesbrough 3-1.
Possebon aliumizwa kwenye dakika ya 66 na Nahodha wa Middlesbrough Emmanuel Pogatetz ambae alipewa kadi nyekundu kwa kosa hilo.
Mechi ilisimama kwa dakika 6 kumtibu Possebon uwanjani na kisha akakimbizwa hospitali alikolazwa usiku mzima na kuruhusiwa asubuhi ilipothibitika hakuvunjika na hakuna madhara makubwa kwenye goti.
Ferguson alifoka: 'Ni rafu mbaya sana na kinachosikitisha ni kuona mchezaji aliefanya faulo analalamika kwamba sio kosa na benchi lake likiunga mkono kuwa sio kadi nyekundu! Afadhali kidogo Meneja wa Middlesbrough Derek Southgate amekubali ni faulo mbaya!'
Possebon ndio kwanza alikuwa anaanza mechi yake ya kwanza kwa Man U.
Nae Nahodha huyo wa Middlebrough Emmanuel Pogatetz sasa atafungiwa kucheza mechi 3 zijazo.

No comments:

Powered By Blogger