Saturday 9 January 2010

Arsenal yashindwa kuipiku Man U kuchukua nafasi ya pili!!
Wakiwa Uwanjani kwao Emirates huku barafu ikidondoka mfululizo, Arsenal ilibidi wajitutumue na kusawazisha mara mbili na kulazimisha sare ya 2-2 na Everton kwenye mechi ya Ligi Kuu.
Katika mzunguko wa kwanza wa Ligi, Arsenal iliisulubu Everton 6-1 Uwanjani Goodison Park nyumbani kwa Everton.
Kwa sare hiyo, Arsenal wamebaki nafasi ya 3 wakiwa na pointi 42 kwa mechi 20, Man U wa pili wakiwa na pointi 43 kwa mechi 20 na Chelsea bado vinara wakiwa wamecheza mechi 20 na wana pointi 45.
Everton walitangulia kufunga dakika ya 12 kupitia Leon Osman na Denilson akaisawazishia Arsenal dakika ya 28 baada ya shuti lake kumbabatiza Osman na kumhadaa Kipa Howard.
Dakika ya 81 Steven Pienaar aliipa Everton bao la pili lakini Arsenal walisawazisha dakika za majeruhi, dakika ya 92, kwa shuti la Rosicky kumbabatiza Beki wa Everton Lucas Neill na kumhadaa Kipa Howard.
VIKOSI:
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Traore, Denilson, Diaby, Ramsey, Nasri, Eduardo, Arshavin.
AKIBA: Fabianski, Rosicky, Vela, Silvestre, Merida, Eastmond, Emmanuel-Thomas.
Everton: Howard, Neville, Neill, Heitinga, Baines, Osman, Cahill, Fellaini, Pienaar, Donovan, Saha.
AKIBA: Nash, Bilyaletdinov, Vaughan, Coleman, Duffy, Baxter, Mustafi.

No comments:

Powered By Blogger