Monday 4 January 2010

Fergie alia, akasirishwa na Timu yake kuanza mwaka vibaya na kutupwa nje ya FA Cup!!!
• Aahidi Fulu Nondo Jumatano na Man City!!
Sir Alex Ferguson amebainisha kuwa aliikemea Timu yake hapo jana mara baada ya kipigo cha 1-0 na Leeds United walichokipata Uwanjani kwao Old Trafford na kutupwa nje ya FA Cup.
Ferguson alipanga Kikosi ‘dhaifu’ mchanganyiko hapo jana kikiwa na Chipukizi Jonny Evans, Fabio, Gibson, Anderson, Obertan na Wellbeck pamoja na Maveterani Garry Neville, Wes Brown na Mastaa Rooney na Berbatov huku Kipa akiwa Kuszczak. Na mwishoni mwa mechi, huku jahazi tayari liko mrama, akawaingiza Owen, Giggs na Valencia.
Jumatano, Man U inakumbana na Mahasimu wao wakubwa Manchester City Uwanjani City of Manchester katika mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling na awali Ferguson alitangaza Chipukizi ndio watacheza mechi hiyo lakini baada ya kipigo kikubwa cha jana, Ferguson ametamka: “Tuna Nusu Fainali Jumatano na Wachezaji wengi waliocheza jana hawatacheza!’
Wadau wanachukulia kauli ya Ferguson, hasa baada ya kuudhiwa na mpira mbovu wa Timu yake hapo jana, ataacha mpango wake wa kuwapanga Makinda na badala yake kuweka Fulu Nondo kama vile Man City wanavyotegemewa kufanya.
Marudiano ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling yatakuwa Old Trafford Januari 19.

No comments:

Powered By Blogger