Saturday 9 January 2010

RATIBA LIGI KUU England: [saa za bongo]
Jumamosi, 9 Januari 2010
Hull v Chelsea [IMEAHIRISHWA]
[saa 12 jioni]
Arsenal v Everton
Burnley v Stoke [IMEAHIRISHWA]
Fulham v Portsmouth [IMEAHIRISHWA]
Sunderland v Bolton [IMEAHIRISHWA]
Wigan vAston Villa [IMEAHIRISHWA]
[saa 2 na nusu usiku]
Birmingham v Man U
Jumapili, 10 Januari 2010
[saa 10 na nusu jioni]
West Ham v Wolves [IMEAHIRISHWA] 
Liverpool v Tottenham [IMAEHIRISHWA]
Jumatatu, 11 Januari 2010
[saa 5 usiku]
Man City v Blackburn
Adebayor asimulia shambulio!!
Nahodha wa Togo, Emmanuel Adebayor, amesema Timu yao Togo itakutana leo ili kuamua kama waendelee kubaki Angola au waondoke kufuatia kupigwa risasi jana kwa Basi lao lililowabeba wakati likitokea Jamhuri ya Congo na kuelekea Cabinda huko Angola kilipo kituo cha Togo kwenye Kundi B la Kombe la Mataifa ya Afrika ambalo wako pamoja na Ghana, Ivory Coast na Burkina Faso.
Katika shambulio hilo Dereva wa basi aliuawa na Wachezaji wawili wa Togo, Serge Akakpo na Kodjovi Obilale pamoja na watu kadhaa, walijeruhiwa kwa risasi.
Adebayor alisema walivuka mpaka wa Congo na Angola salama na kuona Askari wengi wamevalia kivita lakini hilo halikuwastua kwani walidhani ni kwa sababu ya ulinzi mkali kwa ajili ya Mashindano makubwa na wao wakaendelea na safari na walipofika kama kilomita 5 hivi toka mpakani risasi zikaanza kunguruma.
Adebayor akasikitika: “Kuna vitu tunasema na kuvirudia, Afrika lazima tubadilike ili tuheshimiwe lakini hili halitokei!!! Inasikitisha!!! Tuna nafasi ya Mashindano makubwa Duniani, Kombe la Dunia, na unaona kinachotokea? Ni aibu kubwa na si haki!!”
Adebayor akaongeza: “Lakini tunawashkuru askari Walinzi kwani bila wao tungekuwa maiti!! Zilikuwa dakika 30 za mauti!!”
Kufuatia tukio hilo, FIFA imetamka, kupitia Rais wao Sepp Blatter, kusikitishwa na kutoa rambirambi na pole kwa wote waliothirika na vilevile imeahidi kushirikiana na CAF kuchunguza tukio hilo.
CAF imetangaza Mashindano hayo yataendelea Angola kama yalivyopangwa.
Straika wa zamani arudi kama Meneja
Bolton Wanderers wamethibitisha Owen Coyle ambae ni Meneja wa Burnley ndie ameteuliwa kuwa Meneja wao mpya kuchuku nafasi ya Gary Megson aliefukuzwa hivi karibuni.
Oweni Coyle, Raia wa Scotland, amepewa Mkataba wa miaka miwili na nusu na Bolton, Timu ambayo aliwahi kuwa Mchezaji wake hapo zamani.
Uteuzi wa Coyle kuwa Meneja wa Bolton umefikiwa baada ya Klabu za Burnley na Bolton kufikia uamuzi kuhusu kuhama kwake.
Kimsimamo, Bolton wako nafasi ya 18 kwenye Ligi Kuu England na wamemudu kushinda mechi moja tu katika mechi zao 9 za mwisho kwenye Ligi hiyo.

No comments:

Powered By Blogger