Sunday 3 January 2010

Ngoma droo kwa Wababe wa Glasgow!!!
Leo, Uwanjani Parkhead, nyumbani kwa Celtic, Wababe na Mahasimu wa Jijini Glasgow, Scotland, Celtic na Rangers walipambana kwenye mechi ya Ligi Kuu Scotland lakini hakupatikana mbabe na mechi ikaisha 1-1.
Hadi mapumziko, Timu zilikuwa 0-0 na Celtic wakafunga bao lao dakika ya 79 kupitia Scott McDonald lakini dakika mbili baadae Rangers wakarudisha Mfungaji akiwa Lee McCulloch.
Rangers ndio wanaongoza Ligi hiyo kwa kuwa na pointi 44 na Celtic ni wa pili wakiwa na pointi 37 lakini wamecheza mechi moja pungufu.

No comments:

Powered By Blogger