Thursday 7 January 2010

RATIBA LIGI KUU England WIKIENDI HII:
[saa za bongo]
Jumamosi, 9 Januari 2010
[saa 9 dak 45 mchana]
Hull v Chelsea
[saa 12 jioni]
Arsenal v Everton
Birmingham v Man U
Burnley v Stoke
Fulham v Portsmouth
Sunderland v Bolton
Wigan vAston Villa
[saa 2 na nusu usiku]
Birmingham v Man U
Jumapili, 10 Januari 2010
[saa 10 na nusu jioni]
West Ham v Wolves
[saa 1 usiku]
Liverpool v Tottenham
Jumatatu, 11 Januari 2010
[saa 5 usiku]
Man City v Blackburn
Beckham aanza AC Milan kwa ushindi!!!
Hapo jana, David Beckham alianza kuchezea AC Milan kwa mkopo kwa ushindi wa 5-2 dhidi ya Genoa Uwanjani San Siro kwenye mechi ya Ligi Serie A.
Huku Kocha wa England Fabio Capello akiwa miongoni mwa Watazamaji, Beckham alicheza vizuri sana huku akishangiliwa na Washabiki na pengine kumfanya Capello aikubali kauli yake kuwa Beckham alie fiti lazima atakuwa na namba Kikosi cha England kitakachotua Afrika Kusini mwezi Juni kwa Fainali za Kombe la Dunia.
Hata Kocha wa AC Milan, Leonardo, alimsifia: “Ni Mchezaji anaeweza kucheza kokote! Ana kipaji na akili kubwa ya kimbinu mpirani!”
Katika mechi hiyo Ronaldinho alikosa kufunga penalti na Genoa wakapata bao la utangulizi lakini AC Milan wakasawazisha na kuwa mbele 2-1 hadi mapumziko.
Inter Milan ndio vinara wa Ligi Serie A na wako mbele ya AC Milan kwa pointi 8 lakini AC Milan wana mechi moja mkononi.
Inter Milan pia walishinda mechi yao ya Ligi jana walipoifunga Chievo 1-0 kwa goli la Mario Balotelli lakini katika mechi hiyo walipata pigo kubwa baada ya Defenda wao toka Romania Cristian Chivu kuvunjika fuvu kichwani baada ya kugongana vichwa na kulazimika kufanyiwa operesheni ya dharura kichwani.
Madaktari wamesema opersheni hiyo ilienda salama na wana matumaini makubwa Chivu atapona na kuwa salama.

No comments:

Powered By Blogger