Saturday 9 January 2010

LIGI KUU England: Mechi 7 zaganda na barafu!!!
Mechi 7 kati ya 10 zilizokuwa zichezwe wikiendi hii, yaani Jumamosi na Jumapili, hazitachezwa kufuatia barafu na baridi kali iliyoikumba Uingereza na ni mechi 2 tu za leo, Arsenal v Everton na Birmigham v Manchester United, ndizo ambazo zimebaki kwenye Ratiba.
Mechi ya Jumatatu usiku kati ya Manchester City na Blackburn bado haijazungumziwa lolote.
Mechi ambazo hazitochezwa ni:
-Hull v Chelsea
-Burnley v Stoke
-Fulham v Portsmouth
-Sunderland v Bolton
-Wigan v Aston Villa
-West Ham v Wolves
-Liverpool v Tottenham
Tevez na McLeish ni Bora Desemba Ligi Kuu!!
Meneja wa Birmingham, Alex McLeish, na Mchezaji wa Manchester City, Carlos Tevez, ndio Washindi wa Tuzo ya Mdhamini wa Ligi Kuu Barclays kwa Mwezi Desemba ya Meneja Bora na Mchezaji Bora.
Washindi hao wawili ni mara yao ya kwanza kutwaa Tuzo hizo ambazo uamuzi wa kuzizawadia hutolewa na Jopo la Wadhamini hao Barclays ambalo huwa na wawakilishi kutoka Ligi Kuu, FA, Vyombo vya Habari na Mashabiki.
Alex McLeish ametunukiwa Tuzo hiyo, akiwa Meneja wa kwanza wa Birmingham kuipata, baada ya kuiongoza Timu yake kushinda mechi 4 na kutoka sare 2 kwa Mwezi Desemba kwenye Ligi na hivyo kuendeleza wimbi la kutofungwa kufikia mechi 11 mfululizo na kuifikia rekodi ambayo Klabu hiyo ilijiwekea miaka 100 iliyopita.
Nae Tevez ameikwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Desemba baada ya kufunga mabao 7 katika mechi 6 za Ligi.
Hii ni mara ya kwanza kwa Tevez kupata Tuzo hii tangu aanze kucheza Ligi Kuu mwaka 2006 akiwa na West Ham.

No comments:

Powered By Blogger