Thursday 7 January 2010

Straika alieiua Man U ataka kuhama Leeds
Mshambuliaji wa Leeds Jermaine Beckford aliefunga bao moja na la ushindi lililoitupa Manchester United nje ya FA Cup ameiandikia klabu yake ili kuonyesha dhamira yake ya kutaka kuhama huku Klabu kedekede zikimkodolea macho kwa umaarufu alioupata baada ya kuiua Man U.
Beckford Msimu huu ameifungia Leeds mabao 16 katika mechi 21 alizoanza na mwanzoni mwa Msimu aligoma kusaini Mkataba mpya na Leeds.
Kwa vile Mkataba wa Beckford unaisha Mwezi Juni Leeds inabidi wamuuze sasa ili wapate pesa na wakishindwa kufanya hivyo Mwezi Juni ataondoka bure bila Leeds kulipwa chochote.
Inasemekana Newcastle imeshatoa ofa ya Pauni Milioni 1 na nusu kumnunua.
Klabu yenye madeni Pompey italazimika kuuza Wachezaji
Mkurugenzi Mtendaji wa Portsmouth Peter Storrie amesema watalazimika kuwauza baadhi ya Wachezaji wao muhimu ili kuinusuru Klabu hiyo kutangazwa mufilisi.
Habari hizi za kuuzwa Wachezaji zimekuja huku Klabu ikishindwa kulipa Mishahara ya Wachezaji ya Mwezi Desemba ingawa Mkuu huyo ameahidi leo Mishahara italipwa.
Hii ni mara ya tatu kwa Mishahara kucheleweshwa.
Neville: “Tunamtegemea Rooney!”
Nahodha wa Manchester United Garry Neville amekiri Timu yao inamtegemea sana Wayne Rooney katika ufungaji na kuleta ushindi hasa baada ya kuondoka Cristiano Ronaldo.
Rooney Msimu huu amefunga mabao 15 katika mechi 23 alizoanza.
Neville amesema: “Tunamtegemea Rooney. Wayne anatuletea ushindi. Ni Mfungaji Bora Ligi Kuu! Ni mpiganaji na anajituma sana kwenye mechi!”
Man U wako nafasi ya pili kwenye Ligi wakiwa pointi 2 nyuma ya vinara Chelsea na bado wamo kwenye vinyang’anyiro vya Makombe ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Carling lakini wamebwagwa nje ya Kombe la FA.
Neville ameongeza: “Msimu huu Ligi imekuwa ya ajabu! Vigogo wote wamepoteza pointi nyingi! Nadhani ikifika Machi ndio itajionyesha nani ni mgombea Ubingwa wa kweli! Inashangaza tumepoteza mechi 5 lakini tupo pointi 2 tu nyuma ya anaeongoza!”

No comments:

Powered By Blogger