Monday 4 January 2010

KOMBE LA FA: Raundi ya 4 yapangwa, Mechi kuchezwa Januari 23 na 24
Baada ya hekaheka za Raundi ya 3 kupita Jumamosi na Jumapili huku baadhi ya Timu  kushinda na kuingia Raundi ya 4, nyingine kutoka sare na hivyo kulazimika kurudiana na mechi kadhaa kuahirishwa kwa ajili ya kutanda kwa barafu, hatimaye Ratiba ya Raundi ya 4 imetolewa na mechi hizo zinatakiwa zichezwe Wikiendi ya Januari 23 na 24.
Katika Ratiba ifuatayo, zikitajwa Timu 2 ni kwamba Mshindi kati yao hajapatikana na mechi inarudiwa na pia Timu inayotajwa kwanza ndio iko nyumbani.
RATIBA:
Southampton v Ipswich
Reading/Liverpool v Burnley
Millwall/Derby v Brentford/Doncaster
Bristol City/Cardiff v Leicester
Stoke v Arsenal
Notts County/Forest Green v Wigan
Scunthorpe v Man City
West Brom v Plymouth/Newcastle
Everton v Nottm Forest/Birmingham
Accrington/Gillingham v Fulham
Bolton v Sheff Utd/QPR
Portsmouth/Coventry v Sunderland
Preston v Chelsea
Aston Villa v Brighton
Wolves v Crystal Palace
Tottenham v Leeds

No comments:

Powered By Blogger