Sunday 3 January 2010

Meneja Msaidizi wa Man U akiri kipigo ni kikubwa!!!
• Wadau walamikia Fergie kubadili Timu kila kukicha, wengine wahoji siku hizi Man U haina Festi Ilevuni!!!
Baada ya kubwagwa nje ya Kombe la FA leo kwa kipigo cha bao 1-0 na Leeds United ambayo iko Madaraja mawili chini ya Manchester United tena Uwanjani kwao Old Trafford mbele ya Mashabiki 74,000, Meneja Msaidizi wa Man U Mike Phelan amekiri kuwa kipigo hicho ni kikubwa kwao na kukubali kuwa Wachezaji wao hawakujituma kama walivyopaswa na kuwa Leeds United ndio waliocheza kwa kujituma kupita wao.
Phelan pia aliilaumu defensi yao kwa kuruhusu bao laini lilofungwa na Jermaine Beckford dakika ya 19.
Hata hivyo, baadhi ya Wadau wa Manchester United wameulalamikia mtindo wa siku hizi wa Meneja Sir Alex Ferguson wa kubadili Kikosi chake kila kukicha.
Baadhi ya Wadau hao wamesema kwa sasa festi ilevuni ya Man U haijulikana na huwezi hata siku moja ukaotea Wachezaji gani watacheza kwenye mechi.
Hilo, Wadau hao wamesistiza, ndio linafanya Timu siku hizi icheze bila maelewano na mwelekeo.
Mmoja wa Wadau hao alihoji iweje Ferguson kwenye mechi ya leo na Leeds United ambao wana uhasama wa enzi na Man U awapange Chipukizi na wageni wasio na uzoefu wa mechi za mikikimikiki kwa pamoja kama alivyofanya leo kwa kuwaweka kina Fabio, Anderson, Gibson, Obertan na Wellbeck ambao walipwaya mno.
Kwa hilo, Wadau sasa wameanza kuiogopa mechi ijayo ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling itakayochezwa huko City of Manchester Stadium Jumatano tarehe 6 Januari dhidi ya Mahasimu wao Manchester City na woga huo mkubwa unakuja kufuatia kauli ya Sir Alex Ferguson kuwa atachezesha Chipukizi wake kwenye mechi hiyo wakati kila mtu anajua Man City watashuka fulu nondo.

No comments:

Powered By Blogger