Sunday 3 January 2010

KOMBE LA FA MECHI ZA LEO Jumapili, 3 JanuarI 2010
Chelsea v Watford
Man U v Leeds United
Notts County v Forest Green [IMEAHIRISHWA=HALI YA HEWA MBAYA ]
Sheffield United v QPR
Tranmere v Wolves
West Ham v Arsenal
Meneja aliepigwa shoka Bolton aishambulia Klabu hiyo
Garry Megson alietimuliwa kazi ya Umeneja Bolton Wanderers wiki iliyopita ameishutumu vikali Bolton kwa kudai alifukuzwa kinyama.
Megson alidai Mwenyekiti Phil Gartside hakutumia uungwana kwani alimfukuza kwa njia ya simu Jumatano iliyopita.
Bolton wako nafasi ya 18 kwenye Ligi Kuu, hiyo ikiwa ni nafasi ya 3 toka chini, lakini wamecheza mechi chache kuliko Timu nyingine zinazowazunguka.
Megson amesema: “Kwenye Ligi tumecheza mechi chache na tuna mechi mbili mkononi na kama Bolton ikipata pointi mbili kwenye mechi hizo tutakuwa nafasi ya 14! Na, ikishinda mechi moja kati ya hizo mbili, itakuwa nafasi ya 12 nafasi ambayo Bolton hawajahi kufikia kwa miaka mitatu sasa!”
Megson akaongeza na kudai Klabu hiyo kwa sasa ipo kwenye hali bora kuliko alipoingia.
Megson amesema: “Wengi hawajui Klabu hiyo ilikuwa taabani! Wengi wanafikiri ukiingia hapo ni kama kuirithi Real Madrid na mambo yakipinda uko lawamani!”
KOMBE LA FA: Liverpool afueni kwa sare, mechi kurudiwa!!
Jana Liverpool walinusurika kubwagwa nje ya Kombe la FA na Reading baada ya kulazimisha sare ya 1-1 na mechi hii sasa itarudiwa huko Anfield tarehe itakayotajwa baadae.
Reading, ambao wako Daraja la chini ya Ligi Kuu, waliitawala mechi hii na walifunga bao la kuongoza lakini Steven Gerrard akaisawazishia Liverpool.

No comments:

Powered By Blogger