Monday 4 January 2010

KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA: Kunguruma Angola kuanzia Jumapili ijayo!!
Huko Nchini Angola, Nchi 16 za Afrika, wakiwemo Wenyeji Angola na Mabingwa Watetezi Egypt, wataanza kumenyana kuanzia Jumapili ijayo Januari 10 ili kumpata Bingwa wa Afrika.
Nchi hizo 16 zimegawanywa Makundi Manne na zitacheza kwa mtindo wa ligi na Timu mbili za juu toka kila Kundi zitasonga mbele kuingia Robo Fainali.
Mashindano ya kugombea Kombe la Mataifa ya Afrika yalianza rasmi mwaka 1957 na kuchezwa huko Sudan na kushirikisha Nchi 4, Egypt, Sudan, Ethiopia na Afrika Kusini.
Lakini Afrika Kusini wakatolewa hata kabla ya kushirika kwa sababu ya siasa yake ya ubaguzi wa rangi.
Egypt walinyakua Kombe hilo la kwanza walipoifunga Sudan mabao 4-0.
Kuanzia mwaka 1968 Kombe hili limekuwa likishindaniwa kila baada ya miaka miwili.
Katika historia ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Egypt ndio wanaongoza kwa kulitwaa mara nyingi na wamelichukua mara 6.
Ghana na Cameroun wamelitwaa mara 4 kila mmoja.
Congo DR na Nigeria mara 2 kila mmoja.
Nchi zilizolichukua mara moja kila mmoja ni Algeria, Congo, Ivory Coast, Ethiopia, Morocco, Afrika Kusini, Sudan na Tunisia.
RATIBA: KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA ANGOLA 2010
Januari 10:
[KUNDI A]
Angola v Mali
Januari 11:
[KUNDI A]
Malawi v Algeria
[KUNDI B]
Ivory Coast v Burkina Faso
Ghana v Togo
Januari 12:
[KUNDI C]
Egypt v Nigeria
Mozambique v Benini [
Januari 13:
[KUNDI D]
Cameroun v Gabon
Zambia v Tunisia
Januari 14:
[KUNDI A]
Mali v Algeria
Angola v Malawi
Januari 15:
[KUNDI B]
Burkina Faso v Togo
Ivory Coast v Ghana
Januari 16:
[KUNDI C]
Nigeria v Benin
Egypt v Mozambique
Januari 17:
[KUNDI D]
Gabon v Tunisia
Cameroun v Zambia
Januari 18:
[KUNDI A]
Angola v Algeria
Mali v Malawi
Januari 19:
[KUNDI B]
Burkina Faso v Ghana
Ivory Coast v Togo
Januari 20:
[KUNDI C]
Egypt v Benin
Nigeria v Mozambique
Januari 21:
[KUNDI D]
Gabon v Zambia
Cameroun v Tunisia
ROBO FAINALI
Januari 24:
1A v 2B
1B v 2A
Januari 25:
1C v 2D
1D v 2C
NUSU FAINALI
Januari 28:
W25 V w28
W26 V w27
FAINALI
Januari 30

No comments:

Powered By Blogger