Friday 8 January 2010

Barafu yagandisha Mechi Uingereza!!!!
Barafu na baridi kali iliyoshuka hadi viwango chini ya sifuri imesababisha mechi nyingi za Soka na mashindano ya Michezo ya aina mbalimbali Nchini Uingereza kuahirishwa ama kwa vile Viwanja vimeganda barafu au kwa usalama wa Raia kufuatia barabara kufungwa, usafiri kusimamishwa na njia za watu wa miguu kutopitika.
Hadi sasa hakuna mechi za Ligi Kuu England za wikiendi hii zilizotangazwa kuahirishwa lakini mechi kadhaa za Ligi chini ya Ligi Kuu, yaani Daraja liitwalo Championship, zimeahirishwa.
Pia baadhi ya mechi za Madaraja chini ya Championship, yaani Ligi 1 na Ligi 2, zimeahirishwa.
Mechi zilizoahirishwa:
Jumamosi:
Championship: Sheffield Wednesday v Peterborough, Preston v Doncaster, Reading v Newcastle, Watford v Sheff Utd
Tembo wawaua Amavubi
Timu ya Taifa ya Ivory Coast iliyopo maandalizini Bongo kwa ajili ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika yanayoanza Jumapili huko Angola jana waliifunga Rwanda mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Mabao yote ya Tembo yalifungwa dakika 4 za mwisho za mchezo la kwanza likipachikwa na Bamba Souleymane dakika ya 86 kufuatia kona ya Emmanuel Eboue na la pili na Angoua Brou katika dakika za majeruhi.
Katika mechi hiyo Didier Drogba alikosa mabao mengi.
Juzi Tembo waliifunga Bongo 1-0 kwa bao la Drogba.
Ivory Coast wataanza kampeni yao huko Angola kwa kucheza na Burkina Faso Jumatatu.
Hatimaye Wachezaji Pompey wapata Mishahara!!
Baada ya kuchelewa wiki kulipwa Mishahara yao ya Desemba, hii ikiwa ni mara ya 3 kwao kucheleweshewa Mishahara, hatimaye jana Portsmouth iliwalipa Wachezaji wake.
Portsmouth, Timu ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi Kuu England, ipo kwenye balaa kubwa la matatizo ya kifedha na inakabiliwa na kesi ya kutaka kufilisiwa na Mamlaka ya Kodi ya Mapato kwa kushindwa kulipa kodi.
Vilevile, imefungiwa kutonunua Wachezaji kwa kushindwa kulipa madeni ya ununuzi wa Wachezaji toka Klabu nyingine.

No comments:

Powered By Blogger