Wednesday 6 January 2010

LIGI KUU England: Stoke 3 Fulham 2
Katika mechi pekee ya Ligi Kuu iliyochezwa jana usiku huku ikitaliwa na barafu, Stoke City iliibwaga Fulham kwa mabao 3-2 na kutinga nafasi ya 10 ikiwa sasa imecheza mechi 20 na ina pointi 24.
Fulham wako nafasi ya 9 na wamecheza mechi 20 na wana pointi 27.
Mabao yote ys Stoke yalifungwa Kipindi cha Kwanza na Tuncay Sanli, dakika ya 12, Abdoulaye Faye dakika ya 34 na Mamady Sidibe dakika ya 37.
Fulham walicharuka Kipindi cha Pili na kupata bao zao mbili kupitia Damien Duff dakika ya 61 na Clint Dempsey dakika ya 85.
Mancini amtaka Viera
Roberto Mancini anataka ajumuike tena na Patrick Viera na yumo mbioni kumleta Mchezaji huyo Manchester City kutokea Inter Milan ambako kwa sasa hana namba.
Viera, miaka 33, alicheza England akiwa na Arsenal ambako alikuwa Nahodha na kuondoka kuhamia Juventus mwaka 2005 na huko alicheza Msimu mmoja tu na kuhamia Inter Milan wakati huo ikiwa chini ya Roberto Mancini na waliweza kutwaa Ubingwa wa Serie A mwaka 2007 na 2008.
Viera ameichezea Arsenal mechi 400 na kushinda Ligi Kuu mara 3 na Vikombe vya FA mara 4.

No comments:

Powered By Blogger