Thursday 7 January 2010

Straika toka Senegal amkuna Fergie, apewa Jezi ya Tevez!!

Mame Biram Diouf huenda akapata namba muda si mrefu Klabuni Manchester United baada ya Bosi Sir Alex Ferguson kuthibitisha Mshambuliaji huyo Raia wa Senegal anafanya vizuri sana mazoezini.
Diouf, miaka 22, ameshapata kibali cha kazi na tayari Manchester United imeshamkabidhi Jezi Namba 23 iliyokuwa ikivaliwa na Carlos Tevez.
Diouf amesainiwa na Man U kutoka Klabu ya Norway Molde FK Julai 2009 lakini akabakishwa huko huko kwa mkopo kwa vile kulikuwa na utata kuhusu kibali chake cha kazi England.
Ferguson amesema: “Amemudu mazoezi yetu vizuri sana na ametufurahisha! Ni mwepesi, hodari kwa mipira ya juu na mpiga vigongo kweli! Kwa ujumla, ni Senta Fowadi mzuri na atacheza Msimu huu!”

No comments:

Powered By Blogger