Saturday 9 January 2010

KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA: Togo yajitoa!!!
Kufuatia kushambuliwa kwa risasi basi lao walilokuwa wakisafiri nalo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hadi Cabinda, Angola na kuuawa kwa Dereva wa basi hilo na kujeruhiwa kwa Wachezaji wao wawili pamoja na wengine kadhaa kwenye Kikosi chao, Togo imetangaza kujitoa kwenye Mashindano hayo.
Kuna taarifa zisizothibitishwa kuwa mbali ya Dereva wa basi hilo alietangazwa kufariki mara tu baada ya taarifa za shambulio hilo kuzagaa, pia watu wengine wawili ambao hawakutajwa nao wamefariki dunia.
Togo wamepangwa Kundi B pamoja na Ghana, Ivory Coast na Burkina Faso na mechi zao zimepangiwa Mjini Cabinda.
Mpaka sasa CAF imesema Mashindano hayo yataendelea huku ikiitaka Serikali ya Angola iongeze ulinzi.
Waasi wanaotaka uhuru wa Jimbo la Cabinda ambalo ni tajiri kwa mafuta wametangaza kuhusika na shambulio hilo.

No comments:

Powered By Blogger