Tuesday 5 January 2010

Drogba aiua Bongo: Taifa Stars 0 Tembo 1!!
Jana kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam mbele ya maelfu ya Wabongo wakiongozwa na Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, Ivory Coast iliifunga Tanzania bao 1-0 kwa bao lililofungwa na Didier Drogba kwa kichwa baada ya krosi ya Emmanuel Eboue dakika ya 37 ya mchezo.
Ingawa Taifa Stars walifungwa lakini waliweza kumudu kucheza soka la heshima na kuwafanya Tembo hao watumie misuli zaidi ili kuimudu Bongo iliyokuwa ikicheza kitimu na kiakili zaidi.
Ivory Coast wako Dar kwa maandalizi na mazoezi ya kwenda Angola kushiriki Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zinazoanza Nchini humo Januari 10.
Kwenye michuano hiyo, Ivory Coast wamepangwa Kundi B pamoja na Ghana, Burkina Faso na Togo.
Ivory Coast wataanza kucheza mechi yao ya kwanza kwenye Kombe hilo Januari 11 kwa kuvaana na Burkina Faso.

No comments:

Powered By Blogger