Monday 4 January 2010

Meneja wa Burnley azungumza na Bolton ili achukue ofisi!!
Burnley imethibitisha kuwa Meneja wao Owen Coyle yuko kwenye mazungumzo na Bolton Wanderers ili achukue nafasi ya Umeneja iliyo wazi huko baada ya kufukuzwa kazi Garry Megson wiki iliyokwisha.
Coyle, miaka 43, ni Raia wa Scotland aliewahi kuichezea Bolton kati ya 1993 na 1995.
Endapo Coyle atakubaliana na Bolton kuhusu ajira hiyo basi Bolton itabidi wailipe Burnley Pauni Milioni 3 ili wamruhusu ahamie Bolton kwa vile mkataba wake una kipengele cha aina hiyo.
Taarifa zaidi za mazungumzo hayo zitatolewa baadae.

No comments:

Powered By Blogger