Saturday 9 January 2010

Birmingham 1 Man U 1
Leo, Man U wameweza kulazimisha sare ya 1-1 ugenini kwa goli walilojifunga wenyewe Birmingham na hivyo kuikaribia Chelsea kileleni sasa wakiwa pointi moja tu nyuma yao ingawa wamecheza mechi moja zaidi.
Birmingham ndio walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 38 mfungaji akiwa Jerome.
Man U wakasawazisha dakika ya 64 baada ya Beki wa Birmingham Dann kujifunga mwenyewe.
Zikiwa zimesalia dakika 5 mpira kwisha Refa Clattenburg alimpa Kadi ya Njano ya pili Fletcher wa Man U na hivyo kumtoa nje kwa Kadi Nyekundu.
VIKOSI:
Birmingham: Hart, Carr, Roger Johnson, Dann, Ridgewell, Larsson, Ferguson, Bowyer, McFadden, Jerome, Benitez.
AKIBA: Maik Taylor, Martin Taylor, Phillips, Fahey, McSheffrey, Queudrue, Parnaby.
Man Utd: Kuszczak, Rafael Da Silva, Brown, J Evans, Evra, Valencia, Carrick, Scholes, Fletcher, Park, Rooney.
AKIBA: Amos, Neville, Owen, Anderson, Giggs, Fabio Da Silva, Diouf.

No comments:

Powered By Blogger