Sunday 10 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Laanza leo, majonzi na utata vyatawala!
• Hamna uhakika Togo imejitoa au la!!
Leo saa 4 usiku, saa za bongo, Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika yataanza rasmi kwa Wenyeji Angola kucheza na Mali Mjini Luanda, Angola lakini furaha za uzinduzi wa Michuano hii mikubwa Barani Afrika imefunikwa na msiba mkubwa uliotokea baada ya Basi lilobeba Timu ya Togo kushambuliwa kwa risasi muda mfupi baada ya kuvuka mpaka wa Congo na Angola Jimboni Cabinda na kusababisha vifo vya Dereva wa Basi hilo, Kocha Msaidizi na Afisa Habari wa Togo na pia kuwajeruhi Wachezaji wawili.
Awali, Timu ya Togo, ikiongozwa na Nahodha Emmanuel Adebayor, walitangaza kujitoa Mashindanoni lakini leo asubuhi Wachezaji wa Timu hiyo wakatangaza ili kuwaenzi wenzao waliouawa na kujeruhiwa watacheza kishujaa michuano hiyo.
Mara baada ya kuibuka taarifa za Togo kuendelea na Mashindano, Serikali ya Togo ikatoa amri kupitia Waziri Mkuu Gilbert Houngbo kuwa hawaruhusiwi kucheza na lazima warudi nyumbani.
Inasemekana Serikali ya Togo imetuma ndege kuwarudisha Wachezaji wao nyumbani.
Wakati sakata la Togo likiendelea, Serikali ya Angola imeimarisha ulinzi kila kona na ufunguzi rasmi wa Mashindano haya utafanyika baadae leo na kufuatiwa na Mechi ya Kundi A, ambalo limepangiwa Mji wa Luanda, kati ya Angola na Mali.
Katika Kundi A pia wamo Algeria na Malawi.
Mbali ya Mji Mkuu wa Angola, Luanda, michezo mingine ya Makundi mengine imepangiwa kwenye Miji mingine mitatu.
Kundi B la Togo, Ivory Coast, Ghana na Burkina Faso lipo Mjini Cabinda.
Kundi C la Misri, Benin, Mozambique na Nigeria lipo Benguela.
Kundi D la Cameroun, Gabon, Tunisia na Zambia lipo Lubango.
RATIBA KAMILI:
Januari 10:
[KUNDI A]
Angola v Mali
Januari 11:
[KUNDI A]
Malawi v Algeria
[KUNDI B]
Ivory Coast v Burkina Faso
Ghana v Togo
Januari 12:
[KUNDI C]
Egypt v Nigeria
Mozambique v Benini [
Januari 13:
[KUNDI D]
Cameroun v Gabon
Zambia v Tunisia
Januari 14:
[KUNDI A]
Mali v Algeria
Angola v Malawi
Januari 15:
[KUNDI B]
Burkina Faso v Togo
Ivory Coast v Ghana
Januari 16:
[KUNDI C]
Nigeria v Benin
Egypt v Mozambique
Januari 17:
[KUNDI D]
Gabon v Tunisia
Cameroun v Zambia
Januari 18:
[KUNDI A]
Angola v Algeria
Mali v Malawi
Januari 19:
[KUNDI B]
Burkina Faso v Ghana
Ivory Coast v Togo
Januari 20:
[KUNDI C]
Egypt v Benin
Nigeria v Mozambique
Januari 21:
[KUNDI D]
Gabon v Zambia
Cameroun v Tunisia

No comments:

Powered By Blogger